Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mahakama katika Makao Makuu ya Tarafa za Nalasi, Lukumbule na Namasakata – Tunduru?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri sana, na tunaomba waendelee kumalizia hiyo Mahakama. Nina swali moja tu la nyongeza. Kwa kuwa maeneo ya Lukumbule na Masakata na Nalasi yamekosa kabisa huduma za kimahakama: Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuweka Mobile Court katika tarafa hizi ili ziweze kupata huduma za kimahakama? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunashukuru kwa pongezi na shukrani hizo. Kwa sasa Mhimili wa Mahakama una magari mawili (mobile courts) ambazo zinafanya kazi Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Mwanza. Katika bajeti yetu tunategemea kuongeza hizi mobile courts sita Mikoa ya Kagera, Tanga, Dodoma, Arusha, Mara na Morogoro. Tunafanya hivi kwa maeneo ambapo population ni kubwa. Tunatamani tungefika kwa kila Kata, lakini mwenendo wetu wa huu mpango wa Mahakama ni kujenga Mahakama hizo kwa sababu hizi mobile courts ni gharama kuziendesha na wakati mwingine management ya mahabusu na mambo mengine yanaweza yakawa yanaleta gharama kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Kata zake hizi ambazo amezitaja, tutaingiza katika mwaka ujao wa fedha, na tutafikia Kata zake na tutazijenga kwenye maeneo ambapo uhitaji upo, ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mahakama katika Makao Makuu ya Tarafa za Nalasi, Lukumbule na Namasakata – Tunduru?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mahakama ya Wilaya ya Mbulu ni Mahakama chakavu sana iliyojengwa toka enzi za mkoloni; na ni miaka mitatu nimekuwa nikiendelea kuomba ujenzi wa Mahakama hiyo: Je, Serikali ina mpango gani wa kutujengea Mahakama Wilaya ya Mbulu?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Issaay Mbunge wa Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka huu wa fedha, miongoni mwa maeneo tutayokwenda kujenga, tunategemea kujenga Mahakama 18 za Wilaya. Wilaya ya Mbulu ni miongoni mwa Wilaya ambazo tutajenga Mahakama hii. Kweli eneo lao lile, jengo la Mahakama lipo pembeni ya barabara na kimsingi linatakiwa litoke pale. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba huu mpango tunao na tutajenga katika mwaka huu wa fedha. Upo kwenye list yetu. (Makofi)