Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za kuwahifadhi waliofanyiwa ukatili ikizingatiwa kuwa ukatili kwa watoto na wanawake umeongezeka?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa katika mikoa 12 iliyotajwa ya hizo nyumba, Mkoa wa Singida siyo miongoni mwa Mikoa iliyo na hiyo huduma. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha nyumba hizo katika Mkoa wa Singida?

Swali la pili, kwa kuwa ukatili kwa watoto bado unaendelea siku hadi siku. Je, Serikali imefikia wapi au ina mpango gani wa kuanzisha Vituo vya Kulelea Watoto (ECD Centers) ili kuhakikisha kwamba wazazi wanakuwa wanawaacha watoto kwenye mikono salama? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Nehemia Gwau: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kujenga nyumba salama katika Mkoa wa Singida, ni dhahiri kwamba iko mikoa mingi kweli ambayo haina nyumba salama, hapa ni mitano tu inayo, na wizara inafanya jitihada za kuwasiliana na wadau ambao wamekuja kutusaidia katika mapambano haya ya kutokomeza ukatili. Andiko hilo likipita, tutapeleleka hizi rasilimali katika maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa ikiwemo huko Singida.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kupitia mwongozo huu, tunaomba mamlaka za Mikoa na Halmashauri na wadau walioko huko waone umuhimu wa kuanza kuanzisha nyumba hizi wakati Wizara inakuja kuongezea nguvu. Vilevile kwenye bajeti zinazokuja; mwaka ujao tutaendelea kutenga fedha kidogo katika ngazi zote kwa ajili ya kuchochea ujenzi wa nyumba Salama hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu maelezi ya Watoto, ni kweli, mpango wa Serikali ni kuhakikisha watoto wanalelewa vizuri kwa kuwajengea vituo vya kuwalea na kuwakuza katika maeneo ya jamii. Sasa tuna vituo 200 tumeshirikiana na wadau kuvijenga. Formular ni ile ile, tunahamasisha wadau waliopo kwenye Halmashauri zetu waendelee kujitokeza na kuchangia fedha kwa ajili ya vituo hivi, lakini kwenye bajeti zetu tutatenga.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia hivi sasa Wizarani tuna kikao kinaendelea cha resource mobilization. Hivyo, tukiipata, tutaanza kuwapelekea wale ambao wameshamiliki na wameanza huku tukiwaelimisha wengine ambao bado hawajaona umuhimu huo, kuamka na kujipanga kwenye bajeti za mwaka unaokuja, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za kuwahifadhi waliofanyiwa ukatili ikizingatiwa kuwa ukatili kwa watoto na wanawake umeongezeka?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Baadhi ya wahanga wa ukatili wamekuwa wakirushwa picha zao katika mitandao hivyo kutwezwa utu wao; na hivyo kusababisha baadhi ya ambao wanafanyiwa ukatili kutokutoa taarifa: Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na jambo hili?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq kuhusu hao wanaopiga picha mitandaoni, kweli inasikitisha sana. Serikali imekuwa ikitoa maelekezo na maagizo ya kwamba waache kufanya hivyo, na wamekuwa wakiendelea. Sasa kauli ya Serikali ni kwamba, vitendo hivyo ni vibaya katika malezi, makuzi na maadili ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vitendo hivyo vinawaharibu watoto wetu ambao ni Taifa la kesho. Kwa sababu wamekuwa hawasikii, sasa hili ni onyo la mwisho, vinginevyo nakwenda kuita kikao cha wadau wote na wote hao waliopiga hizo picha za namna hiyo, nitaongoza kwenda kuwashitaki kwa mujibu wa sheria kwenye Jeshi la Polisi ili sheria zetu tulizozitunga wenyewe zifanye kazi yake, zisikae tu kabatini. (Makofi)