Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Nyamongo Wilayani Tarime?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa niaba ya watu wa Tarime naomba niishukuru sana Serikali kwa kutenga fedha ya kujenga VETA kule Tarime Vijijini, hasa Nyamongo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; napenda kujua kimetengwa kiasi gani cha fedha angalau chuo kianze kufanya kazi kwa hatua ya mwanzo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; nini kauli ya Serikali kwa wananchi pale ambao wengi ni wachimbaji wadogo wadogo, wavuvi karibu na Ziwa Victoria, lakini pia na wakulima wa mazao mbalimbali na Tarime pia mazao yanastawi. Nini matarajio ya wananchi hasa vijana kwa uwepo wa Chuo cha VETA katika eneo langu? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kujenga vyuo hivi katika kila wilaya kama nilivyoeleza awali. Katika awamu ya kwanza hii ya mwaka 2022/2023 Serikali imetenga bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivyo. Tafsiri yake ni nini, katika kila chuo katika awamu ya kwanza tunapeleka bilioni moja na milioni 400 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa majengo tisa ya awamu ya kwanza. Majengo haya tisa ya awamu ya kwanza yatakapokuwa yamekamilika, vyuo hivi bila shaka vitaanza kufanya kazi ya kutoa huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wetu ni nini? Katika awamu ya pili vilevile tutatenga tena fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo mengine tisa. Jumla kuu ya bajeti yote ili chuo kiweze kukamilika ni jumla ya bilioni tatu na milioni mia tano. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imeweza kutenga katika mwaka huu, lakini vilevile katika mwaka ujao tunakwenda kukamilisha ujenzi huu ambapo vyuo hivi vyote vitakapokamilika ni zaidi ya bilioni 200 tunatarajia kutumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa pili, upande wa mafunzo yatakayotolewa, tunafanya mapitio sasa hivi ya mitaala ile ya utoaji wa mafunzo ya ufundi wa VETA na hasa hasa tutazingatia zile shughuli za kiuchumi zinazofanyika katika maeneo husika. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi kwenye maeneo ya kilimo kutakuwa na mitaala ya kilimo, kwenye maeneo ya madini kutakuwa na mitaala ya shughuli za madini, kwenye maeneo ya uvuvi, tutakwenda hivyo angalau ku-customize kulingana na shughuli za kiuchumi za eneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Nyamongo Wilayani Tarime?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naomba niishukuru Serikali niliomba ituletee vifaa vya kufundishia, walituletea katika Chuo chetu cha VETA, Wilaya, lakini pia niliomba gari na wakatuletea kwa ajili ya utawala, tunawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, kwa kuwa wananchi wamejitokeza kwa wingi, kwa maana kuna wanafunzi wengi katika chuo kile. Je, Serikali inaweza sasa kutuongezea wakufunzi wa masomo mbalimbali wanaosoma pale?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kawawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Kawawa na Waheshimiwa Wabunge wote, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan tayari alishatoa kibali cha kuajiri watumishi wakiwemo wakufunzi pamoja na walimu. Tumepata kibali cha watumishi 571 na mpaka hivi sasa tunavyozungumza watumishi 151 tayari wameshaajiriwa, tutawapeleka Namtumbo na maeneo mengine ya vile vyuo vya zamani, lakini tuna vyuo 25 vipya na vile vinne vya mikoa watakwenda watumishi hawa na tunaendelea kuajiri.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Nyamongo Wilayani Tarime?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Serikali kujenga vyuo vingi vya VETA na ili kuweza kueta hamasa kwa wanafunzi na wazazi kujiunga kwenye vyuo hivi, Serikali ina mpango gani ama mkakati gani wa kutoa mikopo kwa wanafunzi hawa wanaojiunga na Vyuo vya VETA ama vyuo vya kati? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sima, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba, tunatoa mikopo katika elimu ya juu na elimu hii ya kati. Tumetengeneza mkakati huo, lakini kwa mkakati wa muda mfupi tumezungumza na wadau ikiwemo benki na taasisi nyingine za kifedha. Wenzetu wa NMB tayari katika mwaka huu wametoa zaidi ya bilioni 200 kwa ajili ya mikopo katika kada ya hii ya kati ikiwemo na wanafunzi wa vyuo vya VETA na sisi kama Serikali tunatengeneza mkakati. Baada ya mapitio ya mitaala tutajua kitu gani cha kufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Nyamongo Wilayani Tarime?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA, Wilayani Mkuranga, ikizingatia Wilaya ya Mkuranga ni ukanda wa viwanda? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Hawa Mchafu, Mbunge wa kutoka Mkoa wa Pwani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa mchafu na Wabunge wengine wote wa Mkoa wa Pwani. Katika zile wilaya 64 nilizozizungumza awali ipo Wilaya ya Mkuranga, ipo Wilaya ya Kibiti, ipo Wilaya ya Bagamoyo, ipo Wilaya ya Kisarawe. Kazi imeshaanza na shughuli zinaendelea kule Mkuranga na maeneo hayo mengine niliyoyataja kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, kazi tayari imeshaanza. (Makofi)