Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, ni watumishi wangapi wa umma wamefikishwa Mahakamani kwa rushwa, wangapi wameshinda kesi na kurejeshwa kazini kwa kipindi cha 2010 – 2020?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini tunazungumzia maisha ya watu kwa idadi ya watu 863 ambao wameonekana hawana hatia ni asilimia 41.8 ni watu wengi sana katika utendaji wa umma na watu hawa wamepitia mateso, wamedhalilika katika jamii ambayo tunaishi ambapo tuhuma tayari ni uhalifu sasa swali. Serikali inachukua jitihada gani kuwasafisha watumishi ambao wamepelekwa Mahakamani kwa tuhuma za rushwa asilimia 41.8 wameoneka hawana hatia kutumia nguvu ile ile ya kuwatangaza ni wahalifu, wanatumia nguvu gani kuwasafisha watumishi hao? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa madhara ni makubwa ya kisaikolojia, kijamii na haiba yao imechafuka kwenye macho ya umma. Kwa muda gani Serikali itaendelea kuvumilia kuwaona watumishi hawa wanaendelea kuhangaika na nini jitihada za Serikali katika kuhakikisha kwamba wanarudi katika utumishi wakiwa wana haiba njema na safi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Dennis Londo utaratibu wa utumishi wa umma umeelezwa ndani ya sheria kama nilivyozitaja pamoja na sheria nyingine lakini pia utaratibu wa kuwarudisha watumishi kazini nao pia umeelezwa katika sheria hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Dennis Londo utaratibu wa kuwaandikia wale ambao wamekwisha safishwa na Mahakama na kuonekana kwamba hawana makosa utaendelea kufanyika. Pamoja na hilo pia Mheshimiwa Rais, ameelekeza na ndiyo tunayo yafanyia kazi kwamba lazima tuhakikishe kwamba hawa watu ambao wanakutwa hawana makosa tunawafanyia haki la kwanza, lakini pili wanarudishwa kazini mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo lote Mheshimiwa Rais ameendelea kuhakikisha kwamba kupitia Tume yake wa Utumishi wa Umma taratibu na haki zote wa watumishi hawa zinafuatwa na kusimamiwa. (Makofi)