Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, lini TANROADS Mkoa wa Mara wataondoa vigingi katika maeneo ya Wananchi baada ya kushindwa kulipa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, katika maswali ya kuangalia sana ni hili swali. Tumeona Serikali ikiwa ikivamia wananchi kwenye maeneo yaliyovamiwa na Serikali wanabomolewa nyumba zao. Miaka 14 sasa wananchi takriban nchi nzima maeneo yale ambayo ni maeneo nyeti ya barabarani yamekaliwa na Serikali bila fidia, bila kwenda kuyapima. Sasa swali langu lilikuwa linahusu;

Je, ni lini Serikali itatoa tamko la wananchi kung’oa vila vigingi na kuingia kufanya maeneo hayo kwa shughuli za maendeleo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali imesema kwamba maeneo ambayo yamechukuliwa toka 2009 mpaka leo, kuna mengine yatafidiwa kuna mengine kuna hayatafidiwa;

Je, wale ambao hawatafidiwa wako tayari kupewa hela ya usumbufu, kwa maana ya fidia ya usumbufu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, baada ya kuliona hili tatizo katika bajeti ambayo tumepitishiwa ya mwaka huu wa 2023/2024 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kufanya tathmini, na hili linapatikana kwenye ukurasa wa 194 wa kitabu chetu. Tumeeleza hili suala na changamoto yake ambayo ipo. Na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba wale ambao wako ndani ya mita 7.5 nyumba zao hazijabomolewa; ila ziliwekwa alama ya X ya kijani ikionyesha kwamba barabara imewafuata na wanastahili fidia. Kwa hiyo kwa sababu ya nchi nzima ndiyo maana Serikali imekuja kufanya tathmini ione ni maeneo yapi ambayo kweli sasa tutayahitaji na yatafidiwa, na yale ambayo hatutahitaji kwa sasa wananchi wataruhusiwa waendelee kuyatumia baada ya kufanya hiyo tathmini.

Mheshimiwa Spika, hao wa usumbufu nadhani sheria zetu na kanuni zetu za namna ya fidia inavyofanyika zitatumika ili kuona namna ya kuwafidia wale ambao watakuwa wamepata huo usumbufu, ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, lini TANROADS Mkoa wa Mara wataondoa vigingi katika maeneo ya Wananchi baada ya kushindwa kulipa fidia?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika Mkoa wetu wa Lindi barabara zetu kuu na barabara za mikoa zina changamoto hii kubwa ya kuwepo kwa vigingi katikati ya makazi ya wananchi;

Je, ni lini Serikali italipa fidia ili wananchi waendelee na shughuli zao kama kawaida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, suala hili linafanana sana na suala la msingi na jibu langu litaendelea kubaki kwamba; ndiyo maana katika bajeti hii tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya tathmini, na kama ni maeneo ambayo tunayahitaji kwa sasa tutakuja tuwafidie halafu tuweze kujenga hizo barabara ama kuacha hiyo corridor ikiwa wazi baada ya kuwaondoa wananchi kwa kuwafidia likiwa ni pamoja na hilo la eneo la Mheshimiwa Mbunge ambalo amelisema. Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, lini TANROADS Mkoa wa Mara wataondoa vigingi katika maeneo ya Wananchi baada ya kushindwa kulipa fidia?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kuna baadhi ya maeneo unakuta kwamba jiwe la TANROADS limewekwa zaidi ya mita 30 kama ambavyo umetuhabarisha hapo;

Je, katika mazingira hayo TANROADS watakuwa tayari kuondoa mawe hayo kwa gharama zao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama ni barabara ambayo imesanifiwa maana yake ni kwamba pale ilipo ndipo zinapoishia mita 30, na maana yake ni kwamba pale ilipo barabara ambayo ipo itasogea upande huo ili kufikisha mita 30. Hao watakuwa watafidiwa pia kwa sababu barabara itakuwa imehama kutoka ilipokuwa na kusogea upande huo wa kwenye kigingi, ahsante.