Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali yanayoonesha kwamba kikundi kimoja Jimboni Busanda kitapata shilingi milioni 69.4 hivi, ninayo maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Jimbo la Busanda katika maeneo ya Ziwa Viktoria yana vikundi vingine katika Kata ya Nyamwilolelwa, Kata ya Bukondo na Kata ya Nyachiluluma: Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba, inaweza kuongeza vikundi vinavyokopesheka kwenye maeneo hayo ili huduma hii iweze kuwasaidia wananchi wengi kwa ajili ya maendeleo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Nini mkakati wa Serikali kuhamasisha ufugaji wa samaki kwenye maeneo ambayo yako mbali na Ziwa Victoria? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza Mheshimiwa
Mbunge amezungumzia kuhusu kuongeza idadi ya vikundi katika jimbo lake. Bahati nzuri katika mwaka wa fedha tutaongeza idadi ya vikundi kufikia 893. Kwa hiyo, katika mwaka huu unaokuja basi na jimbo lake tutaongeza hivyo vikundi ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameviainisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali kuhusu maeneo ambayo yako mbali na Ziwa Viktoria, ni kwamba, tumeanzisha programu maalum ya ufugaji wa samaki kwa njia ya mabwawa ambayo sasa hivi katika mwaka uliopita tulikuwa na mashamba darasa kumi. Kwa hiyo, matarajio yetu ni kwamba mwaka wa fedha unaokuja, tutafanya hivyo. Kwa hiyo, huo ndiyo mkakati wa sasa na tutaendelea kuhimiza. Mfano mzuri, hata hapa Chamwino tunafanya shamba darasa katika maeneo ambayo ni kame. Kwa hiyo, huo ni mkakati ambao upo na ni endelevu, ahsante sana. (Makofi)

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itatoa elimu kwa wavuvi wa Mkoa wa Mara na hasa wale waliounda vikundi kwa ajili ya ufugaji wa vizimba? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Zoezi la kutoa elimu ni endelevu. Kwa kuwa, vikundi bado viko vingi, basi tutawatuma tena wataalamu wetu waende kuwasaidia wafugaji wa Ziwa Victoria katika Eneo la Mara ambalo Mheshimiwa Mbunge ameainisha, ahsante.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 3

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Buyungu, wapo wafugaji wa samaki ambao wapo katika vikundi, lakini wapo wengine ambao ni mmoja mmoja, lakini wanapungukiwa maarifa na mtaji kwa ajili ya kuwawezesha kufuga kwa tija. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunawawezesha hawa wafugaji waweze kufuga kwa tija? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge. Mkakati wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni pamoja na kuwezesha vikundi mbalimbali vya wavuvi na wavuvi binafsi. Ndiyo maana ukiangalia katika mwaka huu wa fedha tumetoa fedha nyingi na tunaenda kutoa mikopo ya maboti. Kwa hiyo, waliwemo wavuvi wa Jimbo la Mheshimiwa Mbunge, Buyungu kule na wenyewe tutawafikia. Kwa hiyo, tuwaondoe shaka kwenye hilo.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 4

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Nini mkakati wa Serikali wa kuhamasisha wanawake wengi zaidi wafuge kwa kutumia vizimba ili wawezekuepukana na umasikini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan inazingatia sana na imekuwa ikihimiza wanawake kujiunga katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba. Ndiyo maana sasa hivi katika kila programu ambayo tunaianzisha tumeweka pale threshold ambayo lazima kwenye kila program pawepo na wanawake wanaojiunga na shughuli hizo. Kwa hiyo, hiyo ni sehemu yetu na tutaendelea kuisimamia kuhakikisha kwamba wanawake wanaingia katika shughuli hizi, ahsante sana.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Katika Wilaya ya Manyoni tuna kata tatu za Majiri, Maweni na Kijiji cha Kibumagwa ambako kuna uvuvi wa Samaki: Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba, tunaboresha uvuvi huu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Manyoni ambako na kwenyewe wanaendesha uvuvi wa samaki, anachotaka ni sisi kwenda kuboresha. Jukumu letu kubwa ni kwamba, moja, tutaendelea kuleta elimu pamoja na kuongeza vifaa vya kisasa kupitia hii mikopo ya masharti nafuu. Kwa hiyo, tutafika katika kila eneo ambalo watu wetu wanajishughulisha na hizi shughuli za uvuvi pamoja na mifugo, ahsante sana.

Name

Munira Mustafa Khatib

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 6

MHE. MUNIRA MUSTAPHA KHATIB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; je, Serikali ina mkakati gani wa kuvisaidia vikundi ambavyo vilikuwa vimeathirika na kutumia nyavu za wiring?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Vikundi ambavyo vimeathirika na matumizi ya hizo nyavu, kwanza Serikali siyo waumini wa nyavu zile ambazo hazijaruhusiwa nchini. Pili, sasa hivi tumekuwa tukikaa na kampuni zinazotengeneza nyavu kuhakikisha kwamba wanatengeneza nyavu ambazo zime-meet kiwango ili kuondoa vurugu ambazo zimekuwa zikijitokeza na wavuvi wetu kupata hasara. Kwa hiyo, moja ya sehemu ya mkakati wetu ni kuhakikisha kwamba, zana za kisasa zinapatikana kwa wavuvi wetu ili waweze kuvua kisasa, ahsante.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 7

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kule kwetu Mtwara wananchi wamehamasika kufuga majongoo Bahari kwenye vizimba, lakini tatizo kubwa ni vifaranga. Nataka kujua ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha wafugaji wale wanapata vifaranga kwa wakati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, namshukuru sana Mheshimiwa
Mbunge, amezungumzia suala la majongoo bahari ambayo ni moja ya bidhaa kubwa ambayo sisi Wizara ya Mifugo na Uvuvi tunaitangaza. Niwaondoe shaka wananchi wa ukanda ule. Sasa hivi moja ya mkakati wa Serikali, tunaanzisha kituo cha kuzalisha vifaranga katika Mkoa wa Mtwara ili kuhakikisha kwamba uzalishaji wake unakuwa wa haraka na kwa ukaribu zaidi. Kwa hiyo, huo ndiyo mkakati wa sasa na tunalifanya hilo kwa haraka iwezekanavyo.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 8

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba katika ziwa inaonekana ni njia moja nzuri ya kusaidia kupumzisha ziwa kwa wavuvi kuvua katika ziwa. Nini mkakati wa Serikali kusaidia wavuvi katika Ziwa Tanganyika kupata vizimba vya kutosha vya ufugaji wa samaki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Bahati nzuri Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda anajua kabisa mkakati wa Serikali sasa hivi, baada ya kuwekeza sana katika Ziwa Victoria sasa tutafanya hivyo katika Ziwa Tanganyika pamoja na Ziwa Rukwa na Ziwa Nyasa. Ziwa Tanganyika tumeshakaa na Wabunge wa eneo hilo, na mwaka wa fedha unaokuja, mpango wetu kwa asilimia kubwa utakuwa katika ziwa hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha Wavuvi ambao wameunda vikundi na kuanza ufugaji wa vizimba katika Jimbo la Busanda?

Supplementary Question 9

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kule Mufindi Kusini kuna Mabwawa ya Nzivi, Ngwazi pamoja na Kihanga; na mabwawa mengine kama yale ya Ihoanza ambayo yanachimbwa. Changamoto kubwa ambayo ilikuwepo pale ni mambo mawili; suala la vifaranga takribani milioni tano na zana za uvuvi: Je, Serikali iko tayari kupeleka vifaranga takribani milioni tano pamoja na mikopo ya vifaa vya uvuvi vya kisasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Uzuri ni kwamba, jambo hili ambalo amelizungumza Mheshimiwa Kihenzile, alishafika mpaka ofisini kwetu na tulizungumzanaye mimi pamoja na Mheshimiwa Waziri na wataalamu wetu. Tulishamuahidi kwa sababu, kwa sasa tuna vifaranga kama milioni 15 na tuliahidi katika jimbo lake kupeleka minimum ya vifaranga milioni nne. Kwa hiyo, hilo lipo katika mpango, ikiwemo zana za kisasa kulingana na tutakavyovipata katika mwaka wa fedha unaokuja, ahsante.