Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri hayo ya ndugu yangu Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali haijali kuona mashine zile zimekaa kwenye makasha ya kusafirishia kwa miaka saba kuwa zinaweza kuharibika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali ina ushauri gani juu ya wagonjwa wanaokaa kusubiri huduma za x-ray mashine na ultrasound ili kufanyiwa upasuaji, ukizingatia kuwa hata katika hospitali ya Wilaya iliyoko kilomita tano tu kutoka Upuge nako huduma hizi hazipatikani kwa sababu mtumiaji wa mashine hizo hayupo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Maige kama ifuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inajali sana na ndiyo maana kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi fedha ilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo yaliyokuwapo mwanzo, lakini nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge ndani ya wiki hii nitaomba mbele ya Bunge lako tukufu, niongozane naye na wataalam wa afya kufika katika Kituo cha Afya cha Upuge na kuona ni namna gani tunaweza kuchukua hatua kwa sababu haikubaliki miaka saba vifaa hivi vikakaa bila kutumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili nirejee kwenye jibu langu la kwanza katika maswali yake ya nyongeza. Tutatatua changamoto hizi tukiwa site palepale na Mheshimiwa Maige, lakini nikiwa katika ziara hiyo kwa sababu kuna Mbunge mwingine wa Tabora ambaye alizungumzia basi tutatembelea pia Kituo cha Afya cha Misha kuhakikisha tuone changamoto zilizopo na kuhakikisha tunazitatua. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nataka kujua tu ni lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya kukamilisha Kituo cha Afya cha Kisaki? Pia ikikupendeza Mheshimiwa Waziri wakati unaenda Tabora upitie Singida uzungumze na wananchi wa Singida pale Kisaki. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema Mheshimiwa Sima tutapokuwa tunaelekea Tabora basi tutahakikisha tunapita Manispaa ya Singida ili kuona kituo hiki cha Kisaki na tutafanya maamuzi tukiwa pale kadri ya bajeti itakavyoruhusu.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana. Kwa kuwa huduma ya ultrasound imekuwa na umuhimu wa kipekee kwa wakinamama wajawazito.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuweka huduma hiyo ya ultrasound katika vituo vya kliniki ya mama na mtoto? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni adhma ya Serikali hii ya awamu ya sita kuhakikisha kwamba inakuwa ina vifaatiba vya kisasa katika vituo vyetu vyote vya afya hapa nchini. Tutahakikisha kwamba kadri miaka inavyokwenda na bajeti inatakavyoruhusu tunatenga fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya ultrasound kwenye maeneo yenye wodi za mama na mtoto kama ambavyo Mheshimiwa Kisangi amezungumza.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Swaya ni Kata ambayo iko pembezoni sana. Je, ni lini Serikali itaamua kujenga kituo cha afya maeneo yale katika Wilaya ya Rungwe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakagenda kuhusu kata ya Swaya, ninatoa agizo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha anafika katika Kata hii na kufanya tathmini, kuona ni namna gani kama kuna zahanati pale basi iweze kuombewa kupandishwa hadhi na maombi hayo yaletwe Ofisi ya Rais - TAMISEMI ili tuweze kuyachakata na baada yakipandishwa hadhi tutafutie fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ni lini Serikali itapeleka majokofu kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti kwenye vituo vya afya vya Muriti na Bwisya Jimboni Ukerewe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya majokofu haya katika vituo vya afya kule Ukerewe alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge kadri ya upatikanaji wa fedha na tutaangalia katika bajeti hii tunayoenda kuitekeleza ya 2023/2024, kama imetengwa fedha tutahakikisha inafika mara moja kwa ajili ya kupunguza changamoto hii iliyopo katika Wilaya ya Ukerewe.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 6

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimshukuru Mheshimiwa Rais ametupa fedha za x–ray mashine 150,000,000 katika Kata ya Sirari ambayo inahudumia Bumera, Mwema, Susuni Sirari, Kanyange, Itiryo, Mbuguni, Pemba na Ganyange.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua x–ray mashine ipo pale hakuna ukaguzi wa mataalam wa mionzi na hakuna mtaalam, hawa wananchi wanapata shida. Nini kauli ya Serikali katika jambo hili? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hii x–ray iliyopo Kata ya Sirari pale, tuna timu ambayo ni ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI inayozunguka nchini kote kutoa mafunzo kwa wataalam wetu wa afya namna ya kutumia vifaa hivi vya kisasa. Sasa nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako tukufu kuelekeza timu ile iweze kufika Mkoani Mara na kufika Sirari kwa ajili ya kutoa mafunzo ili x–ray hii mashine iweze kuanza kutumika mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara ya mwisho timu hii ilikuwa Mkoa wa Simiyu, kwa hiyo siyo mbali kutoka Mkoa wa Simiyu na kuweza kufika Sirari kwa ajili ya kutoa mafunzo haya ili wananchi waweze kupata huduma.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga vyumba maalum vya kuweka mitambo ya x–ray na ultra sound katika Kituo cha Afya Upuge?

Supplementary Question 7

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hospitali ya Wilaya ya Hai x–ray mashine ni ya muda mrefu sana na ni chakavu na imekuwa ikiharibika mara kwa mara.

Je, ni lini Serikali itatununulia x–ray mashine mpya kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Hai?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amekuwa hili pia akilifuatilia sana la x–ray mashine Wilaya ya Hai, tutaangalia katika mwaka wa fedha huu 2023/2024 kama fedha imetengwa na kama haijatengwa basi tutaangalia katika mwaka wa fedha 2024/2025 kuhakikisha kwamba wananchi wa Hai wanapata x–ray mashine basi Serikali iweze kutenga fedha hizo katika 2024/2025.(Makofi)