Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: - Je, zimebaki changamoto ngapi za Muungano kutatuliwa baada ya kufanyika jitihada za kuzipunguza?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wakati mwingine kusuasua kwa utekelezwaji wa changamoto inapelekea kuibuka kwa changamoto mpya za Muungano. Ni nini commitment ya Serikali kuweza kuzuia changamoto yoyote nyingine ya Muungano isijitokeze?

Swali langu la pili, Serikali inatoa commitment gani ya kutatua changamoto hizi nne zilizobakia? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nikianza na swali la kwanza la Mheshimiwa Mbunge namna ya kuzuia changamoto nyingine mpya zisijitokeze, hili ni juhudi ya Serikali zote mbili kuhakikisha wakati wote mara baada ya maamuzi yale yanayojitokeza katika vikao vile vya majadiliano vilivyotatua ile migogoro kuanza utekelezaji mara moja wa yale makubaliano waliyofikia.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, hizi changamoto nne zilizobaki mkononi tunatarajia kwamba kikao chetu kitakuwa mwezi wa Agosti, ambapo katika mazingira ya kawaida hizi zilizobaki ni chache sana tunaweza tukafika mahali, Mungu jalia tutazimaliza zote nne na watu tutaanza kufaida matunda ya Muungano wetu. Ahsante.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: - Je, zimebaki changamoto ngapi za Muungano kutatuliwa baada ya kufanyika jitihada za kuzipunguza?

Supplementary Question 2

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa kero za Muungano zina zungumzika, Je, vile vikao vya Wizara moja moja baina ya SMT na SMZ ambao hukaa kuzungumza kero zao bado vinaendelea au vimefunikwa na hivyo vikao vikubwa?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza kwa msingi wa mazungumzo ya utatuzi wa migogoro hii ambayo iko kati yetu, kitu cha kwanza kabisa ni Wizara zile zenye matatizo yanayosababisha tukasoma kama tatizo kuu kukutana mara kwa mara, kwa sababu hawa ni kama Technical Committee ambazo zinatafuta majibu kwa ajili ya kupeleka kwenye kile kikao kikuu. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunaendelea na vikao vya Wizara kati ya Wizara na Wizara. Kwa mfano, katika haya yaliyobaki Wizara ya Fedha Zanzibar na Wizara ya Fedha Tanzania Bara wanaendelea kuchakata mambo mbalimbali ambayo mwisho wa yote yatatuletea majibu ya utekelezaji. Ahsante.