Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga hospitali kubwa katika Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza. Bukoba Government Referral Hospital haijafikia hadhi ya kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera. Hata Mheshimiwa Waziri wa Afya alisimama hapa na yeye mwenyewe akakiri kwamba ile hospitali bado haijafikia ile hadhi, na mkatuahidi kwamba mtatuletea fedha kusudi tuweze kujenga hospitali nyingine au kukarabati ile ifikie hadhi hiyo: Je, ni lini Serikali italeta fedha za kutosha kuweza kutuhakikishia kwamba wanatujengea hospitali yenye hadhi ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Mkoa wa Kagera uko mpakani na unapakana na nchi kadhaa. Kwa hiyo, yakitokea magonjwa ya mlipuko ni rahisi kuingia Mkoa wa Kagera kwa sababu magonjwa hayana mipaka. Kwa kuwa juzi juzi uliingia mgonjwa mbaya sana wa Marburg na mkaona Wizara na Mkoa walivyokuwa wanahangaika kutafuta mahali pa kuweka wale watu waliokuwa wamechangamana na wagonjwa, kwa sababu hakuna isolation centers ikabidi wawaweke mpaka kwenye mahoteli na hayo mahoteli yakafungwa yakawa hayatoi huduma kwa wakati huo: Je, ni lini sasa Serikali itaujengea Mkoa wa Kagera Isolation center? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufatiliaje wake makini wa masuala ya afya ya Mkoa wake wa Kagera. Pia nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea, hata mwaka huu inatarajia kupeleka zaidi ya shilingi bilioni nne kwa ajili ya kuendelea kuboresha hospitali yao ya Mkoa. Vile vile nimhakikishie kwamba hospitali ya Mkoa wa Kagera ni sawa na Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, level yake ni moja, lakini tutaendelea kuwaongezea wataalam na vitu vingine ambavyo vimepungua kwenye hospitali yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, Mheshimiwa Mushashu anazungumzia suala la ugonjwa wa Marburg. Nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumeshapata heka 90 ndani ya Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kujenga hiyo isolation center. Wakati huo tunapojenga isolation center tunahitaji tafakuri ya kina, kwa sababu ninyi Wabunge wa Mkoa wa Kagera mnajua kuna mwenzetu, Dkt. Mahona Ndulu wakati akihudumia wagonjwa wa Marburg alipata matatizo ya figo na moyo ambapo ilihitaji awepo kwenye sehemu ambazo hizo huduma zitakuwepo. Wakati tunatafakari hayo, tutaendelea kuona namna gani tutaitumia hiyo sehemu ya heka 90.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Wabunge wa Mkoa wa Kagera kwa nia yao ya kwenda kumpongeza daktari huyo.