Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika nakushukuru. Kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii ya uchumi, ni nini hasa mkakati wa Serikali kuhakikisha inajenga barabara hii kwa haraka?

Swali langu la pili, Jimbo la Mtwara Mjini lina changamoto kubwa sana ya barabara; je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuliangalia jimbo hili kwa jicho la tatu ili iweze kulijengea barabara nyingi za lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua umuhimu wa barabara hii kama Serikali na ndiyo maana tumeshafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na tunahakikisha ya kwamba barabara hii inapitika kila mwaka. Katika mwaka wa fedha ujao imetengewa takribani shilingi milioni 188.435 na katika mwaka ujao pia tutafanya usanifu wa kina ili iwe maandalizi katika kujenga katika kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, barabara katika Mkoa wa Mtwara hususan Mtwara Vijijini na Mjini, Serikali inatambua umuhimu wa barabara kuboreshwa katika Mkoa huo. Ndiyo maana hivi sasa kuna miradi ile ya EPC + Financing, kuna barabara ambazo pia ziko katika Mkoa wa Mtwara na ambazo hivi karibuni tutaenda kusaini mkataba kabla ya mwezi wa sita mwaka huu, 2023, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Barabara ya Mbulu – Karatu – Haydom – Sibiti mliahidi kujenga kwa kiwango cha lami na kipande hiki cha Mbulu – Haydom, Mheshimiwa Waziri uliahidi utasaini mkataba kabla ya bajeti yako Jumatatu. Hebu tuambie leo na uwambie wananchi wa Mbulu, mkataba huo utasaini lini?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia sana suala la barabara hii na wewe ni shahidi kwamba Mheshimiwa Mbunge, katika Bunge lililopita alipiga sarakasi kuhusiana na suala hili la barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi chini ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni Sikivu. Sasa, tunakwenda kusaini mkataba kesho na tutasaini pale Haydom. Kwa hiyo, niwatangazie wananchi wa jimbo hili kwamba kesho ni siku muhimu kwao katika kushuhudia kusainiwa mkataba wa ujenzi wa barabara hii. Hongera sana Mheshimiwa Mbunge, kwa kufuatilia barua hii.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara ya Singida – Ilongero hadi Haydom upembuzi yakinifu umekwishafanyika; je, Serikali itakamlisha lini barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekwisha kamilika na sasa Serikali inatafiuta fedha ili tujenge kwa kiwango cha lami barabara hii, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Kufuatia ujenzi wa bandari ya uvuvi unaoendelea pale Kilwa Masoko. Nini mpango wa Serikali kupanua barabara ya kutoka Kilwa Masoko mpaka Nangurukuru ili iweze kukidhi haja ya wakati wa sasa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli pale Kilwa Masoko tunajenga bandari ya kisasa ya uvuvi na katika mipango yetu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia TANROADS, tutaboresha pia barabara hii kutoka eneo la bandari ri kwenda katika eneo la pale mjini na kwa maana hiyo Mheshimiwa Mbunge katika mwaka wa fedha ujao barabara hii tumeitengea fedha kwa ajili ya kuboresha katika ujenzi wa kiwango cha lami. Ni sehemu ya mradi huu wa uijenzi wa hii Bandari ya Kilwa Masoko, ahsante.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 5

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya kutoka Igawa kuelekea Mbeya inapita Jimbo la Makete. Ni barabara yenye volume kubwa ya magari na inachangia uchumi wa Tanzania kwa kiwango kikubwa sana. Je, ni ipi commitment ya Serikali ili iweze kujenga barabara hii ambayo pia anaitumia Mheshimiwa Spika na imekuwa ni nyembamba kwa kiwango ambacho inahatarisha sana usalama wa wapitaji wa barabara ile? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii aliyoitamka ya Igawa kwenda Makete inapita milimani na ni barabara muhimu sana katika uchumi wa wananchi wa maeneo hayo. Pia amesema kwamba ni barabara ambayo Mheshimiwa Spika anapita. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa maeneo hayo kwamba, hii barabara ni miongoni mwa barabara ambazo ziko kati ya huu Mradi wa EPC + Financing kuanzia Igawa – Mbeya mpaka Tunduma.

Mheshimiwa Spika, barabara nyingine ambazo zinakwenda kusainiwa, kwa ridhaa yako naomba nizitaje hapa ili Waheshimiwa Wabunge wasipate nafasi ya kuwa na mashaka.

(i) Ifakara – Malinyi – Lumecha hadi Songea;

(ii) Igawa - Mbeya – Tunduma;

(iii) Karatu – Haydom – Mbulu – Sibiti hadi Maswa;

(iv) Mafinga – Mgororo;

(v) Masasi – Nachingwea – Liwale;

(vi) Kongwa – Kibaya – Arusha; na

(vii) Handeni – Kiberashi – Chemba - Kwa Mtoro hadi Singida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara hizi zitasainiwa mwezi wa sita, na tumshukuru sana Mheshimiwa Rais, katika historia ya nchi hii tunakwenda kusaini kilometa zaidi ya 2000 na Mheshimiwa Waziri alikwisha tamka akiwa pale Singida.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 6

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Nilitaka nimuulize tu Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini sasa mtakuja Kiteto kusaini mkataba wa hii barabara ya Kongwa – Kiteto mpaka Arusha?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hii ni miongoni mwa barabra ambazo nimezitamka hapa kwamba zitasainiwa kabla ya mwezi wa sita. Barabara ambazo ziko katika EPC+ Financing, ahsante.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kuelekea Msimbati?

Supplementary Question 7

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kutokana na umuhimu mkubwa wa kiuchumi na shughuli za kijamii kwa wananchi wa Ngoreme hasa upande ule wa Majimoto, Busawe na Iramba. Ni lini sasa barabara ya Musoma kutoka pale makutano ya Nyakanga mpaka Sirori Simba kupitia Iramba - Majimoto mpaka Nyasirori itajengwa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitamka Mheshimiwa Mbunge, ni barabara ambayo katika mwaka huu wa fedha tulikuwa tumeifanyia upembuzi yakinifu wa awali na katika mwaka wa fedha ujao tutaifanyia upembuzi yakinifu wa kina kama maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.