Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na majibu ya Serikali. Naomba kutumia nafasi hii kwanza kuipongeza Serikali, kwa maana ya Wizara ya Kilimo na Wizara ya Wizara ya Mambo ya Nje kwa programu hii ya kuwajengea vijana uwezo na mafunzo ya ziada, na pia kuipongeza Serikali hususan Wizara ya Kilimo kwa kuwajumuisha hawa vijana 79 katika programu ya BBT. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Kwa kuwa vijana hawa tayari walishasoma vyuo vikuu na vyuo vya kati na wakapata ujuzi wa ziada huko Israel; je, Serikali kwa maana ya Wizara ya Kilimo iko tayari sasa pamoja na kuwahusisha kwenye BBT kuanzisha hiyo programu ya mashamba makubwa (block farming); na kwa kuwa tayari wenyewe ujuzi wanao; na tayari hawa 79 wanatumika kule lakini hawa waanze kabisa kazi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu Serikali imetenga fedha nyingi na inajenga miradi mingi ya umwagiliaji ambayo bila shaka itahitaji wataalam katika kuiendesha katika kuwasaidia wakulima wetu; je, Serikali iko tayari kuwatumia baadhi ya vijana hawa kwa mfumo hata wa kuwalipa japo posho ya kujikimu ili wawasaidiwe wakulima wetu katika hii miradi mikubwa ambayo imetekelezeka hususan kule Mtura?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cosato Chumi kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza vijana wote ambao wanaenda Israel kwenye sekta ya kilimo mazao, wapo wengine ambao hawaendi kwenye sekta ya kilimo mazao; wengine wanaenda kwenye mifugo na maeneo ya namna hiyo. Kwa hiyo, wale ambao wako kwenye sekta ya kilimo mazao, tumeanza kuwa- incorporate kwenye programu ya BBT kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi. Wapo ambao tayari wanafanya shughuli za kilimo ambapo tumeanza kuwatambua sasa hivi, wanafanya shughuli za uzalishaji katika maeneo yao na tumewaingiza kwenye component ya pili ya programu ya BBT ya kuwapa grants na mikopo nafuu ya asilimia 4.5. Kwa hiyo, tumeshaanza kuwatambua na kuwaangalia.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuwatumia kama extensional officers, nilitaka tu niliambie Bunge lako tukufu kwamba, kuanzia mwaka ujao wa fedha na tutakapoleta mabadiliko ya Sheria ya Umwagiliaji na Ugani hapa ndani ya Bunge lako, tunaangalia namna ya kuwatumia vijana waliopo mashuleni kwenye programu za extension ambao wanafundishwa katika vyuo vyetu vya kilimo. Vile vile vijana ambao wana utaalam wa kilimo ili kuanza kuanzisha kampuni binafsi za extension services kwa wakulima na waweze kutoa huduma za namna hiyo.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kupata nafasi. Naishukuru Serikali kwa majibu. Je, Serikali haioni kuwa sasa shule zetu za sekondari za kata zimekuwa na wanafunzi wengi wasiopata kuendelea na masomo ya juu na kwa hiyo, vijana hao wangekuwa sehemu moja ya kuwajengea uwezo wale wanafunzi walioko shuleni kwa kuanzisha mashamba madogo ya majaribio na mafunzo katika shule hizo katika kanda na wilaya zetu? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sasa hivi kuna mchakato unaendelea wa mapitio ya sera ya elimu, nami naishukuru Wizara ya Elimu kuweza kuchukua component ya agriculture kuwa sehemu ya mapitio haya ya sera. Mawazo kama haya tutaendelea kuyapokea na siwezi kutoa commitment sasa hivi kwamba tutaanza kuweka mashamba darasa katika kila sekondari, lakini ni wazo na ninashukuru, nasi kama Serikali tumelipokea.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa mafanikio makubwa ya kilimo Israel ni yale ya Kibbutz Farms na vijana wa kitanzania waliofanikiwa nadhani hayo ndiyo pia wanaenda kujifunza: Je, Serikali iko tayari sasa kutumia vijana hao kuwarejesha katika maeneo yao ya vijijini kwa sababu Watanzania wengi na karibu wote ni wakulima wadogo wadogo ili wanufaike?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mama Shally Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye majibu ya msingi na maswali aliyouliza Mheshimiwa Cosato, namna ya kuwatumia vijana hawa ni lazima tuwe na mfumo wa ugharamiaji kwa sababu huwezi kutaraji kumpeleka kijana kijijini ukamwambie akatoe elimu bila kuwa na mfumo wa ugharamiaji.

Mheshimiwa Spika, tumepokea mawazo ya Waheshimiwa Wabunge na wadau wengi wa sekta ya kilimo namna ya kuwatumia vijana walioenda Israel, walioenda nje lakini wapo vijana ambao wamesoma katika vyuo vyetu, wamesoma kilimo na wana utaalam wa kilimo cha kisasa, lakini bado wapo mtaani. Kwa hiyo, kama Wizara, tunapoenda kupitia mapitio ya sheria ambayo tutaileta ndani ya Bunge lako tukufu ya Irrigation and Extension Services, tuta-incorporate component ya vijana ambao wana elimu ya extension namna ambavyo watatumika na namna gani tutakuwa na mfumo mzuri wa ugharamiaji wa huduma zao.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Wilaya ya Kahama haijanufaika na mradi wa BBT; na kwa kuwa Halmashauri ya Msalala sasa tuko tayari kupokea mradi huu kwa vijana wetu: Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri utafika katika Halmashauri ya Msalala ili tuweze kuanzisha mradi huu? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Wizara iko tayari kushirikiana na Halmashauri yoyote katika nchi yetu ambayo iko tayari kutenga eneo la kilimo kwa ajili ya mfumo wa block farm na kwa ajili ya mfumo wa BBT. Mfano mzuri ni Halmashauri ya Makete ambao wameamua kutenga ten percent yao kuwakopesha vijana, na sisi Wizara tukawapatia pembejeo kwa maana ya mbegu za bure kwa ajili ya kilimo cha ngano. Kwa hiyo, nihamasishe Waheshimiwa Wabunge ninyi ni wajumbe wa Baraza la Madiwani, ni wajumbe wa Kamati za Fedha tengeni maeneo na kuwa tayari kutenga sehemu ya asilimia kumi za Halmashauri kuwasaidia vijana katika maeneo yenu, na Wizara tuko tayari kuja ku-support initiatives za namna hiyo. (Makofi)

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Supplementary Question 5

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa nchi yetu imejaliwa wahitimu wengi wa vyuo vikuu kila kona wakiwemo kule Nachingwea. Je, Serikali inachukua vigezo gani kuwapeleka

hawa vijana wetu ambao wametapakaa nchi nzima huko Israel? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, cha kwanza hii programu inakuwa coordinated na Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na taasisi ya Ministry Affairs ya Israel for International Development and Corporation. Mara nyingi Serikali huwa inatoa window na huwa kuna utaratibu maalum ambao unatumika namna ya kuwapata vijana wanao-apply na kuweza kwenda kushiriki katika windows za namna hii.

Mheshimiwa Spika, tumekutana na ubalozi wa Israel hivi karibuni na kujadiliana nao namna ya kuboresha huduma ya kuwapata vijana, kwa sababu wapo vijana ambao wana apply kwa ajili ya kwenda kufanya jambo A, wakifika kule wanajikuta wamekuwa committed kufanya jambo lingine tofauti na kile ambacho walitarajia. Tumeongea na Ubalozi wa Israel, tunaendelea nao na mazungumzo tukishirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje, badala ya kuwasafirisha hao vijana. Tunavyo vituo vingi katika nchi yetu. Ushirikiano ule wa utalaam tuweze kuutumia ndani ya nchi na waweze kuja kutusaidia ndani ya nchi yetu. (Makofi)