Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, kwa kiasi gani ushiriki wa Tanzania katika mikutano ya Kimataifa unazingatia upatikanaji wa fursa za kiuchumi na utekelezaji wake?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali na kwa kutambua jitihada kubwa ambazo anaweka Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha diplomasia ya kiuchumi, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Je, Serikali haioni ipo haja ya kufanya mapping katika nchi za nje ili kujua katika kila nchi tunataka kuwauzia nini na pia kujua kutoka kila nchi sisi tunataka kuwauzia nini ili tuweze kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na sekta binafsi na pia kuziwezesha balozi zetu za nje kuweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi pamoja na balozi za nje hapa nchini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Wizara ya Mambo ya Nje iko tayari kuandaa mfumo ambao utaweza kufanya tracking ya utekelezaji wa mafanikio yaliyoainishwa yanayotokana na ziara ya viongozi wetu kimataifa, kwa sababu utekelezaji wake haufanywi moja kwa moja na Wizara hii ya mambo ya nje, bali unafanywa na Wizara nyingine pamoja na taasisi nyingine? Ahsante.

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, kwanza nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kusaidiana na sekta binafsi katika kufanya mapping ya fursa ambazo zipo katika nchi mbalimbali huko nje. Napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Wizara ya Mambo ya Nje inafanya kazi kwa karibu sana na sekta binafsi. Kwanza sekta binafsi pia hushiriki katika ziara za viongozi wetu mbalimbali huko nje, ambapo Wizara hizo huwafungulia milango na kujua fursa mbalimbali za uwekezaji. Pia kupitia mabalozi wetu wa nchi mbalimbali, tumekuwa tukiwaunganisha na sekta binafsi ili kujua fursa mbalimbali ambazo ziko huko.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la ufuatiliaji wa yatokanayo na safari za viongozi wetu, hili ni suala muhimu sana, nasi tuna wajibu sana wa kufuatilia kwamba ziara za viongozi wetu zinaleta matunda ipasavyo. Hivyo, uko mfumo maalum wa kuhakikisha kwamba sekta zote ambazo zinaguswa na ziara hizo tunakaa pamoja, tunafanya mkutano na kuainisha utekelezaji wake ili kujua changamoto na faida zake ili kupatiwa ufumbuzi ipasavyo, ahsante sana.