Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, kiasi gani cha bajeti kimetengwa TARURA miaka mitatu mfululizo kwa ajili ya ukarabati wa barabara Kyerwa na upi ufanisi wake?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mpaka sasa barabara za vumbi ni zaidi ya asilimia 70 na barabara ya lami ikiwa ni asilimia 0.4 na changarawe asilimia 29.

Swali la kwanza, ni kwa nini bajeti imeendelea kuwa kidogo, ambayo ni shilingi bilioni tatu, wakati barabara za vumbi na za udongo bado ni zaidi ya asilimia 70?

Swali la pili, ni lini itatengenezwa barabara ya kutoka Kyerwa kwenda STAMICO ambako kuna biashara kubwa ya madini ya bati, ni lini barabara itatengenezwa, sambamba na kuunganisha Kata ya Mabira na Kata ya Kibale?

Mheshimiwa Spika, naomba majibu.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetoa maelezo katika majibu yangu ya msingi, bajeti imeendelea kuongezeka ndani ya miaka hii mitatu. Ukiangalia trend mwaka wa fedha 2020/2021 bajeti katika Wilaya ya Kyerwa ilikuwa shilingi bilioni 1.26 tu, lakini hivi tunavyozungumza bajeti hiyo imekwenda mpaka shilingi bilioni 3.18 kwa maana imeongezeka mara mbili ya vile ilivyokuwa 2020/2021.

Mheshimiwa Spika, hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuiboreshea nchi yetu barabara zake za vijijini na mijini kupitia Wakala wa Barabara (TARURA). Kwa hiyo, nikutoea mashaka Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kuweka fedha kuangalia ni namna gani barabara hizi zinatengenezwa.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la barabara hii ya Kyerwa – STAMICO kupitia Kata ya Mabira na kadhalika, tayari katika kiwango cha lami tulianza kwa kujenga kilometa mbili kwenye Mji Mdogo wa Nkwenda, kuna barabara ambayo ipo kutoka Kido Hospitali katika Mji wa Kyerwa, vilevile tutakwenda sasa kuangalia hii kwenye bajeti zijazo tuweze kutenga fedha kwa ajili ya barabara hii ya Kyerwa mpaka STAMICO.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, kiasi gani cha bajeti kimetengwa TARURA miaka mitatu mfululizo kwa ajili ya ukarabati wa barabara Kyerwa na upi ufanisi wake?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali kuendelea kuongeza bajeti kwenye barabara za TARURA Wilayani Kyerwa.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kasoni kwenye Kata ya Nyakatuntu kwenda mpaka Mkuyu Kata ya Kikukuru niliiombea fedha na fedha imeshapatikana.

Je, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha changarawe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Kasoni – Nyakatuntu – Mkuyu kwa maana imetengewa fedha kwenye bajeti hii ambayo tunaanza kuitekeleza tarehe 1 Julai mwaka huu, tutahakikisha kwamba barabara hii inapatiwa mkandarasi haraka ili iweze kuanza kujengwa.

Mheshimiwa Spika, ninapongeza jitihada za Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Bilakwate, kwa maana amekuwa akiifuatilia sana barabara hii na kuhakikisha kwamba inatekelezwa kwa wakati. (Makofi)