Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini shule za Sekondari Nyamtukuza, Muhange, Shuhudia, Kasanda na Gwanumpu zitakuwa za kidato cha tano na kidato cha sita?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kabla sijauliza maswali naomba niweke kumbukumbu sawa ni Shule ya Sekondari Gwanumpu na Shule ya Sekondari Shuhudia. Baada ya masahihisho hayo ninashukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kakonko inayo shule moja tu ya sekondari ambayo ni Shule ya Sekondari Kakonko, na katika majibu ya Serikali amebainisha kwamba Shule ya Sekondari Muhange inapungukiwa mabweni mawili tu.

Je, lini sasa Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kujenga hayo mabweni mawili ili masomo yaweze kuanza pale?

Swali la pili, amebainisha shule hizi za Sekondari Shuhudia, Kasanda, Nyamtukuza na Gwanumpu zinapungukiwa miundombinu mbalimbali, lakini kinachohitajika hapo ni fedha. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba miundombinu hii inayopungua inakamilika na masomo yaweze kuanza katika shule hizi? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la kwanza la lini fedha itakwenda kukamilisha mabweni haya ambayo tayari yameshaanza kujengwa. Serikali itapeleka fedha kadiri ya upatikanaji wake na tutaangalia katika bajeti hii iliyopitishwa ya mwaka wa fedha 2023/24 kuona kama hiyo shule imetengwa fedha, kama haijatengewa tutajitahidi tuitengee fedha 2024/2025.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili kuhusu Shule za Gwanumpu, Shuhudia na Nyamtukuza ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, tutaangalia vilevile kuona uwezekano wa kuzitengea fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.