Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, kwa kiasi gani vijana wa Mtwara wamenufaika na programu ya kukuza ujuzi?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza: -

Je, Serikali iko tayari kufanya tathmini kwa vijana hao ambao wamepatiwa mafunzo ya uanagenzi katika Mkoa wa Mtwara na nchi nzima ili kuona kama hiyo programu ina tija?

Swali la pili, hao vijana ambao hawajapatiwa vyeti kwa maana ya kutambuliwa ama kurasimishwa, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba vijana hao wamepatiwa vyeti na kutambulika katika elimu isiyo na mfumo rasmi? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iko tayari kufanya tathmini na siyo kwa Mkoa wa Mtwara pekee, ni nchi nzima kwa sababu sera hii ni kwa ajili ya wananchi wote.

Mheshimiwa Spika, kwa kipengele cha pili, wale ambao wamekidhi vigezo vya kupatiwa vyeti, utaratibu utafwatwa na watapatiwa vyeti vyao. Ahsante. (Makofi)