Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Daraja la Mto Wami ni miongoni mwa daraja la muda mrefu na jembamba (single way). Aidha, daraja hilo limesababisha ajali za mara kwa mara na kusababisha wasafiri kupoteza maisha na mali zao:- Je, ni lini Serikali itajenga daraja jipya katika Mto Wami hasa ikizingatiwa kuwa daraja hilo ni kiunganishi kati ya Dar es Salaam na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kutokana na changamoto za daraja la Wami kufanana sana na changamoto za madaraja ambayo yanaunganisha barabara inayotoka Handeni kwenda Turiani, je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa madaraja haya ili barabara inayounganisha Handeni na Mkoa wa Morogoro iweze kufanya kazi na kupitika? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoongelea Mheshimiwa Mboni Mhita pamoja na madaraja ambayo yamo katika barabara hiyo ni sehemu ya barabara iliyotolewa ahadi na viongozi wetu wa Kitaifa ijengwe kwa kiwango cha lami. Nami naomba nimhakikishie, tupo hapa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambapo kazi yetu kubwa ni moja tu kuwajengea miundombinu Watanzania kwa kuhakikisha kwamba ahadi zote za viongozi wetu wakuu zinatekelezwa. Pamoja na kwamba madaraja haya na barabara hii kama alivyoona katika bajeti tuliyoipitisha haikuwekewa fedha ya kutosha, nimhakikishie baada ya kukamilisha madaraja na barabara ambazo tayari wakandarasi walikuwa site kuanzia Awamu ya Nne, tutaanza kushambulia ahadi ambazo zilitolewa na viongozi wetu na ahadi zote zilizopo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba tunazikamilisha katika miaka inayofuata.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Daraja la Mto Wami ni miongoni mwa daraja la muda mrefu na jembamba (single way). Aidha, daraja hilo limesababisha ajali za mara kwa mara na kusababisha wasafiri kupoteza maisha na mali zao:- Je, ni lini Serikali itajenga daraja jipya katika Mto Wami hasa ikizingatiwa kuwa daraja hilo ni kiunganishi kati ya Dar es Salaam na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Umuhimu wa kimkakati wa daraja la Wami kwa maana ya usalama wa nchi yetu na uchumi wa Taifa letu unafanana sana na umuhimu wa kimkakati wa barabara ya Mabokweni - Maramba - Bombo Mtoni - Mlalo -Same kwa maana ni barabara inayopita kwenye maeneo ambayo ni mpakani, kwa hiyo, ina umuhimu wa kiusalama. Vilevile ni barabara ambayo inaunganisha mbuga za wanyama na inaunganisha Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Kilimanjaro. Je, Serikali kwa umuhimu ule ule wa kimkakati, ipo tayari sasa kuijenga kwa kiwango cha lami barabara hii?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni bahati mbaya kwamba Mheshimiwa Mbunge alipofika ofisini kuleta tatizo la barabara hii au tuseme umuhimu, changamoto ya barabara hii, tuliongea lakini hatukumalizia kwa sababu kulikuwa na mambo mengine yalituvuruga. Mimi naomba sana tukae tena tumalizie ile kazi ya kuijadili hii barabara kwa undani tukiwashirikisha wataalamu wetu ili hatimaye tuwatendee haki wanaotumia hii barabara.

Name

Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Daraja la Mto Wami ni miongoni mwa daraja la muda mrefu na jembamba (single way). Aidha, daraja hilo limesababisha ajali za mara kwa mara na kusababisha wasafiri kupoteza maisha na mali zao:- Je, ni lini Serikali itajenga daraja jipya katika Mto Wami hasa ikizingatiwa kuwa daraja hilo ni kiunganishi kati ya Dar es Salaam na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa kututengea fedha kwenye barabara ya Mbuyu wa Mjerumani Mbulu ambapo ina daraja la Magara ingawa fedha hiyo ni kidogo na imetengwa katika maeneo matatu au manne. Wabunge wa Babati na Mbulu tukishirikiana na Mheshimiwa Issaay na Mheshimiwa Flatei, tumekuwa tunaomba ile fedha yote iliyotengwa mwaka huu shilingi milioni 300 kama inawezekana na tumeshawasilisha kwa uongozi wa Mkoa, iende kujenga daraja la Magara ambapo itaonyesha mafanikio badala ya kuitumia katika maeneo mengine. Tunaomba Wizara itukubalie tupeleke fedha hiyo kwenye daraja na likikamilika basi hayo maeneo mengine yaendelee kufanyiwa kazi.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Jitu, ingawa siyo sahihi ni Jitu Soni lakini kule wanasema Mbunge wetu ni Jitu lakini nadhani wana maana ya umakini unaotumia katika kufuatilia mahitaji yao. Nampongeza sana kwa hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu hili halimhusu yeye pake yake, linamhusu Mheshimiwa Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini na Waheshimiwa Wabunge wengine kama watatu hivi. Naomba kuwahakikishia kwamba ombi lenu tumelipokea, tutalitafakari na tutalifanyia kazi.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Daraja la Mto Wami ni miongoni mwa daraja la muda mrefu na jembamba (single way). Aidha, daraja hilo limesababisha ajali za mara kwa mara na kusababisha wasafiri kupoteza maisha na mali zao:- Je, ni lini Serikali itajenga daraja jipya katika Mto Wami hasa ikizingatiwa kuwa daraja hilo ni kiunganishi kati ya Dar es Salaam na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini?

Supplementary Question 4

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kuipongeza sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa ujenzi wa daraja la Igumbilo ambalo leo hii wakimbiza mwenge wanalizindua pale katika Jimbo la Iringa Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kuhusiana na ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Dodoma - Mtera - Iringa ambao umekamilika lakini sasa kuna malori makubwa sana yanakatiza katikati ya mji na kusababisha msongamano na barabara hii kuharibika katikati ya mji. Ni lini sasa ule mchepuko ambao ulikuwa umetengwa, ambao unatokea kwenye Chuo cha Tumaini kwenda kwenye barabara kuu utakamilika kwa sababu sasa hivi magari mengi sana yanapita kwenye ile barabara? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa mzito wa Iringa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mchepuo wa Iringa upo katika mipango yetu. Naomba nimhakikishie kwamba kile ambacho wao kwa maana ya RCC walikileta kwetu na sisi tumekichukua, tutakifuatilia kuhakikisha kwamba tunakitekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini? Naomba tu Mheshimiwa Mbunge anipe nafasi kwa sababu siyo sahihi sana kutamka tarehe hapa, lakini naomba aangalie dhamira yetu kwamba ni ya dhati na tutatekeleza mradi huo wa ujenzi wa mchepuo wa barabara pale Mjini Iringa.