Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha Uwanja wa Ushirika Moshi ili kukuza utalii wa michezo nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, pamoja na Serikali kutenga fedha za ukarabati kila mwaka, lakini vyumba vya kubadilishia wachezaji ni chakavu, pia chumba cha marefarii kipo karibu sana na chumba cha timu pinzani ambayo inaleta wakati mwingine sintofahamu. Je ni lini sasa Serikali inaweza kutatua changamoto hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je nini mpango wa Serikali kuongeza nguvu katika kujenga Uwanja wa Majengo ambao unajengwa kwa fedha za ndani ili uweze kukamilika mapema? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Malleko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishaeleza katika majibu ya swali la msingi kwamba ni wajibu wa Serikali kupitia Chuo chetu cha Ushirika kwa maoteo ya bajeti kwa ajili ya ukarabati. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na nilithibitishie Bunge lako Tukufu tutaendelea kufanya hivyo na hivi sasa tutatupia macho maeneo hayo aliyoyataja katika vyumba hivyo vya kubadilishia nguo pamoja na hiki chumba cha marefarii, tutafanya hayo marekebisho labda katika bajeti ijayo ya fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, anataka kufahamu vile vile mkakati wa Serikali kuhusiana na Uwanja huo wa Majengo. Naomba nimthibitishie Mbunge kwamba uwanja huo tunafahamu kwamba uko chini ya Manispaa ya Moshi. Kwa hiyo tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI, lakini vile vile Wizara yenye dhamana ya michezo kuhakikisha kwamba tunatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha Uwanja wa Ushirika Moshi ili kukuza utalii wa michezo nchini?

Supplementary Question 2

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri Mbunge wa Segerea, Mheshimiwa Bonnah hajapata majibu na anasumbuliwa sana na wananchi kuhusu Uwanja wa Sigara Tabata, Jimbo la Segerea. Hebu nenda kalifuatilieni hili, mtuambie nani anayemiliki ili mumsaidie Mbunge aweze kuwaambia wananchi wake.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, tumelipokea.