Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kukomesha vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hali ya ukatili nchini hapa ni mbaya bado hususani kwa wanawake na watoto. Kwanza niwapongeze umoja wa wanawake Tanzania kwa kuweza kufatilia ufanisi wa madawati ya kijinsia nchi nzima. Lakini vilevile madawati haya bado yanachangamoto kubwa sana ikiwemo ukosefu ya miundombinu rafiki ya kuhudumia wahanga hawa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka mazingira rafiki ya kuboresha miundombinu hii ili kuulinda usiri wa wahanga hawa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni juzi tu kuna kesi ya ulawiti mzazi kamlawiti mtoto wake Mkoani Shinyanga na kesi hii imepelekwa Mahakani juzi. Tukio hili limetokea Januari lakini kesi imepekwa juzi, mtuhumiwa huyu amepewa dhamani.

Je, Serikali haioni licha ya ushahidi wote uliyopelekwa Mahakani lakini mtuhumiwa huyu kapewa dhamani; je, Serikali haioni kwamba kwenye kulegeza mazingira haya ya kesi hizi inachochea mazingara haya kwenye jamii zetu? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, madawati mengi yalianzishwa kwa kutumia majengo ya zamani ndani ya vituo vya polisi. Hata hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jensi la Polisi ili kuboresha madawati hayo lakini hata hivyo hadi sasa madawati 79 yenye viwango yameisha jengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili; kosa la ubakaji na ulawiti ni makosa ambayo yanadhaminika kisheria hivyo watuhumiwa kuachiwa huru na kupewa dhamana haimanishi Serikali ina halalisha na kuchochea ongezeko na vitendo vya ukatili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupitia Bunge lako Tukufu kama kuna vifungu vya sheria ambavyo mnahisi vinaleta msongamano kwa wananchi ama vinaleta tatizo basi Waheshimiwa Wabunge mlete maoni yenu ili Wizara ya Katiba na Sheria iweze Kutunga Sheria na kutafuta…

NAIBU SPIKA: Ahsante kwa majibu mazuri, ahsante sana.