Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Simbo - Kalya yenye urefu wa km 234?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hiyo barabara ya Simbo – Kalya, hiyo barabara inaendelea mpaka Wilaya ya Tanganyika ambayo ni Kalya -Lugalaba, Bujombe yenye urefu wa kilometa 37 ambayo inaenda kwenye Wilaya ya Tanganyika katika Mkoa wa Katavi. Ni lini nayo itawekewa fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha changarawe?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika barabara hiyo hiyo, iko barabara ambayo ni ya Lukoma hadi Mwese, yenye urefu wa kilometa 47 ambayo nayo inakwenda nayo kwenye Mkoa wa Katavi. Naomba nijue, ni lini nayo itawekewa fedha kwa ajili ya ujenzi? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambazo tunazihudumia sisi zinaishia Kalya, lakini ni kweli pia kwamba, kwa sababu tumeshawekeza eneo la Sibosye, tuna bandari yetu pale, kwa hiyo, tumefungua barabara mpaka Sibosye kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hiyo bandari inafanya kazi, na tutaendelea kwa barabara ambayo inaenda Katavi. Pia kwa upande wa Kigoma tumeshaifungua mpaka mpakani mwa Katavi, na wenzetu wa Katavi pia wameshaanza kutenga fedha kuifungua ili hizo barabara ziweze kuunganishwa ambapo itatumika pia kama barabara ya ulinzi kwa mikoa hiyo miwili ya Katavi na Mkoa wa Kigoma, ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Simbo - Kalya yenye urefu wa km 234?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kipande cha barabara ya lami kutoka Mbulu Garbabi, kazi ya Mkandarasi imesimama kwa miezi minne; je, ni lini mkandarasi yule ataanza kazi ile rasmi ili barabara hiyo iweze kutekelezwa kwa wakati na kwa mujibu wa mkataba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoisema hii, ni kweli kulikuwa kuna changamoto ya mvua na pia mkandarasi alikuwa hajalipwa fedha zake alizokuwa anadai. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunavyoongea sasa hivi mkandarasi ameshaanza kazi ya Mbulu kwenda Garbabi na tunategemea muda wowote kuanzia sasa tutasaini mkataba wa Labay kwenda Haydom, ahsante.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Simbo - Kalya yenye urefu wa km 234?

Supplementary Question 3

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Tunaishukuru sana Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi kwa kusukuma sana ujenzi wa barabara ya Sanzate – Nata; je, ni lini kipande cha Nata mpaka Mugumu ujenzi wake utaanza? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Nata kwenda Mugumu ni barabara ambayo tutakuwa tunakamilisha barabara ya makutano Nata hadi Mugumu. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti ambayo tunaiendea, tumeipanga ili iweze kukamilika na hivyo kukamilisha mzunguko wa Nata – Mugumu; Mugumu hadi Tarinya kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Simbo - Kalya yenye urefu wa km 234?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mlowo – Utambalila mpaka Kamsamba, nyaraka za tenda, usanifu wa kina, kila kitu kipo tayari, na ipo ndani ya mpango wa bajeti: Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili ujenzi wa kiwango wa cha lami uanze kwenye hiyo barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mlowo - Utambalila hadi Kamsamba, barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa anaiulizia mara kwa mara, tumemhakikishia kwamba hiyo barabara ambayo inaunga Mkoa wa Songwe na Rukwa, tumeiweka kwenye mapendekezo, na tuliagizwa pia na viongozi kwamba barabara hiyo sasa tuanze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tusubiri bajeti kama itapitishwa, barabara hiyo tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.