Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza kutoa Posho kwa Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi ya maswali ya nyongeza. Nitakuwa na maswali mawili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali haina utaratibu maalum wa ulipaji wa posho kwa hawa Wenyeviti wa Mitaa, Vitongoji na Vijiji na wamejitengenezea utaratibu wa kujipatia fedha kupitia mihuri yao na uuzaji wa viwanja kitu ambacho kinaleta migogoro mingi sana kwenye jamii na kaadhia kubwa kwenye jamii na urasimu mkubwa.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na utaratibu maalum wa kuwa na posho ya madaraka kwa viongozi hawa wa ngazi ya mitaa, vijiji na vitongoji? (Makofi)

Swali la pili, Wenyeviti hawa wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji pamoja na Madiwani wamekuwa na dhamana kubwa sana ya usimamizi wa miradi ya Serikali kwenye maeneo yao, lakini mpaka leo hawana posho ya usimamizi wa miradi.

Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kunakuwa na posho ya usimamizi wa miradi kwenye maeneo yao? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwandabila.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza la Serikali haina utaratibu maalum na ni nini kauli ya Serikali kuweka utaratibu huo. Kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba kwa mujibu wa Sheria ile ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Sura Namba 290, posho hizi zinatakiwa zilipwe kutoka kwenye mapato ya ndani ya Halmashauri husika na ndiyo maana Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuziimarisha hizi Halmashauri zetu kwa kuwapa miradi ya kimkakati kuwajengea vyanzo vya mapato mbalimbali ambavyo vitaongezea nguvu kuweza kulipa posho hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili ya usimamizi wa miradi. Ni kweli Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji, Mitaa wanafanya kazi nzuri katika kusimamia miradi, hasa miradi mingi ambayo kwa sasa tumeona Taifa letu Mheshimiwa Rais amemwaga miradi katika Sekta mbalimbali. Nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kulileta hili hapa na tunalichukua kama Serikali kwa sababu lina budget implication na pale ambapo tutaona Serikali ina uwezo wa kuweka kwenye bajeti zake tutaweka lakini kwa sasa bado tutaendelea na utaratibu ule kama sheria inavyotaka ile ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Sura Namba 290.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza kutoa Posho kwa Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa, Serikali imezipokea halmashauri kulipa ile posho iliyokuwa ya Madiwani.

Je, sasa Wizara haioni kwa nini isielekeze zile posho zilizokuwa zinalipwa kwa Madiwani na Halmashauri ziende zikawalipe Wenyeviti wa Serikali za Vijiji? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, hili nalipokea kwa niaba ya Serikali na tutakwenda kuliangalia na kulifanyia kazi na kama tutaona liko viable basi tutachukua hatua.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza kutoa Posho kwa Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji?

Supplementary Question 3

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Serikali katika Bajeti yake ilipitisha posho ya Watendaji wa Kata ya kila mwezi, lakini posho hii imeonekana ni hisani. Baadhi ya Halmashauri zinalipa zingine hazilipi.

Je, Serikali mna tamko gani kuhusu posho hizi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, posho hizi zilipitishwa kwenye bajeti na Bunge hili Tukufu na tutaenda kuhakikisha kwamba linatekelezwa kwa sababu tayari zilitengwa ili Watendaji hawa waweze kupata posho hizi za madaraka.