Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka walimu wa kike katika shule za sekondari na msingi – Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kumuuliza Mheshimiwa Waziri, maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali, lakini ni ukweli usiofichika kwamba mazingira ya walimu wetu kwa maeneo ya vijijini ni tofauti kabisa na maeneo ya mjini. Sasa kumekuwa na upungufu mkubwa wa walimu wa kike kutokana na mazingira hususan kwenye halmashauri ama majimbo ama wilaya za vijijini.

Swali langu la kwanza; je, ni lini Serikali itaanza kulipa posho kwa ajili ya mazingira magumu kwa walimu wetu Tanzania, hususan wa kike? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kutokana na upungufu mkubwa wa walimu, Wilaya ya Chemba tuna shule zaidi ya sita ambazo wanafunzi wameshindwa kuendelea na masomo, hatuna walimu. Shule hizo ni Shule ya Magarasta Sanzawa, Mialo Kwa Mtoro, Hanaa Gwandi, Magandi Soya, Mkandinde Soya pamoja na Lugoba Kata ya Kimaha.

Je, ni lini Serikali itapeleka walimu hawa ili watoto wetu kwenye shule hizi sita waanze masomo ili na wao waweze kutumiza haki yao ya kikatiba? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA YA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge; swali lake kwanza la mazingira, Serikali hakuna incentive maalum ya mazingira na hivi sasa Serikali inaandaa mwongozo kwa ajili ya posho ya masaa ya ziada. Incentive kubwa ambayo inatolewa na Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kwamba inaweka mazingira bora kwa kujenga nyumba, kutengeneza miundombinu ya barabara, kuvuta umeme kwenye vijiji vyote vya nchi yetu hii ambayo nayo inatengeneza mazingira bora kwa watumishi wetu kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge la maeneo haya ambayo ni Sanzawa, Gwandi, Soya ni lini yapata watumishi. Kama nilivyosema hapo awali Serikali imetangaza ajira zaidi ya 21,000 ambapo katika ajira hizi za Walimu na maeneo haya yaliyotajwa nayo yatapata. Nimueleze tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ajira za mwaka uliopita, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ndio ilipata Walimu wengi zaidi wa kike katika Mkoa huu wa Dodoma.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka walimu wa kike katika shule za sekondari na msingi – Chemba?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mkoa wa Simiyu una upungufu sana wa walimu kwa upande wa sekondari na shule ya msingi. Walimu wa kike ni wachache sana na shule zingine hazina kabisa walimu wa kike.

Je, Serikali ina mpango kutuletea walimu wa kike katika Mkoa wa Simiyu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA YA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tayari Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilishatoa maelekezo kwa Makatibu Tawala wote wa mikoa ya Tanzania Bara. Kuhakikisha wanafanya msawazo katika shule zilizo ndani ya mikoa yao na kupeleka walimu wa kike na wakiume katika maeneo ambayo hayana.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii ya Bunge lako tukufu kwa Niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kumwelekeza RAS wa Mkoa wa Simiyu kuhakikisha anafanya msawazo na kupeleka walimu katika shule ambazo hazina Walimu wa kike wa kutosha.