Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Serikali imepanua wigo wa uandishi na usomaji wa vitabu vya ziada na kiada mashuleni na kuna wakati tunapokea vitabu mbalimbali kutoka kwa wahisani. (a) Je, ni utaratibu gani uliopo wa kudhibiti vitabu visivyo na maadili mema kwa watoto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Kitengo cha Udhibiti na Usimamizi wa Vitabu?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwanza, nilitaka nifahamu kwa wale waandishi na wachapishaji ambao wamechapisha vitabu vyenye maadili mabovu au wametoa taarifa za uongo kupitia vitabu hivyo wamepewa adhabu gani?
Pili, ninataka kujua kwa kuwa wananfunzi wanaotoka Visiwa vya Unguja huwa wanafanya mitihani ya Kitaifa sambamba na wenzao wa Tanzania Bara; je, Wizara inafanya utaratibu gani kuhakikisha kwanza mihtasari na vitabu kwa maana ya mitaala na vitabu inawafikia wanafunzi wa Zanzibar mapema ili na wao waweze kujisomea na kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi vitabu vyote kabla ya kupitishwa vinatathminiwa na baada ya kutathminiwa, vinaangaliwa katika suala la maadili inayoendana katika misingi ya kwamba huyu mwanafunzi atafundishwa vipi. Lakini vilevile siyo maadili tu hata uchapishaji wake kitabu kilivyochapishwa kinaleta uhalisia wa yale yanayokusudiwa kufundishwa au laa! Kwa mfano, kama tuna lengo la kumfundisha mtoto kwamba haya ni mayai, basi tunategemea kwamba na kitabu hicho hata picha itaonyesha mayai ambayo ni meupe na itaonyesha kweli yale ni mayai, hayataonyeshwa mayai wakati hapo imechorwa embe. Kwa wanaokuwa hawajatekelza wajibu wao ipasavyo vitabu hivyo vinakuwa haviruhusiwi kupelekwa au kusambazwa au kuchapishwa kwa maana hiyo wanatakiwa kurekebisha hayo makosa. Hayo yalishafanyika hata katika vitabu ambavyo sisi wenyewe tulikuwa tukivishughulikia na tulivizuia visiweze kuendelea.
Pili; kwa upande wa Zanzibar kimsingi Zanzibar wao wanayo mamlaka yao ya elimu ambayo inashugulikia masuala yote hayo ya mitaala pamoja na vitabu. Lakini kwa kuwa sisi wote ni ndugu na tuna masuala ya ushirikiano wa kielimu huwa pia tunaweza kusaidiana katika masuala ya kitaalam lakini pia hata kuchukua best practice katika kutoka upande wowote wa nchi kwa faida ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, ningependa kuongezea kidogo majibu mazuri aliyoyatoa Naibu Waziri wa Elimu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nataka nitoe tu ufafanuzi kuhusiana na mitaala ya elimu ya sekondari kwa upande wa Zanzibar. Kama alivyoelezea Mheshimiwa Naibu Waziri kwa upande wa elimu ya msingi mitaala inatengenezwa na upande wa Zanzibar, lakini kwenye upande wa sekondari mitaala inatengenezwa na Taasisi ya Elimu Tanzania ambayo utaratibu ni shirikishi wakati wa mitaala inapotengenezwa tunawashirikisha upande wa Zanzibar na vilevile hata katika Bodi ya Taasisi ya Elimu Tanzania kunakuwa na uwakilishi wa Wajumbe wa kutoka Zanzibar.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na utaratibu wa usambazaji wa vitabu ili vifike Zanzibar kwa wakati, utaratibu ni kama unavyotumika Bara kwamba kwanza zoezi ni shirikishi la vinapokuwa tayari Wizarra ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar huwa inafanya hilo jukumu.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Serikali imepanua wigo wa uandishi na usomaji wa vitabu vya ziada na kiada mashuleni na kuna wakati tunapokea vitabu mbalimbali kutoka kwa wahisani. (a) Je, ni utaratibu gani uliopo wa kudhibiti vitabu visivyo na maadili mema kwa watoto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Kitengo cha Udhibiti na Usimamizi wa Vitabu?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa shule zetu nyingi bado zinaendelea na utaratibu wa matumizi ya vitabu vingi vya kiada; na kwa kuwa vitabu hivi vimekuwa vikitofautiana kwenye baadhi ya maudhui yaliyomo kwenye vitabu hivi na kuleta mkanganyiko kwa wanafunzi. Je, lini sasa Serikali itaanza kutekeleza utaratibu wa kutumia kitabu kimoja nchi nzima ili kuleta usawa na kuondoa mkanganyiko wa wananfunzi hao?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa baada ya Serikali pamoja na wananchi kugundua kwamba kuna vitabu vingi ambavyo vinatumika mashuleni kiasi cha kushindwa kutoa mwelekeo halisi hasa katika usimamiaji wa maarifa yanayopatikana, Serikali iliamua kwamba kuwe na vitabu vya kiada na ziada, mpaka sasa imekuwa inasimamia katika zoezi hilo la upatikanaji wa hivyo vitabu kadri ya fedha tunavyozipata. Hivyo naamini tukishakuwa tumekamilisha hali hiyo ya kuwa na vitabu ambavyo ni vya aina tofauti tofauti itaondoka.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Serikali imepanua wigo wa uandishi na usomaji wa vitabu vya ziada na kiada mashuleni na kuna wakati tunapokea vitabu mbalimbali kutoka kwa wahisani. (a) Je, ni utaratibu gani uliopo wa kudhibiti vitabu visivyo na maadili mema kwa watoto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Kitengo cha Udhibiti na Usimamizi wa Vitabu?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
16
Kwa kuwa hapo awali Serikali ilikuwa na chombo ambacho kinadhibiti education materials yaani EMAC na kwa kuwa ilivunjwa rasmi huko nyuma na kutamka kwamba wataunda chombo kingine kwa ajili ya kudhibiti vifaa vinavyoingia katika mfumo wa elimu pamoja na vitabu.
Je, Serikali inaukakasi gani wa kuunda chombo hicho maana mpaka leo hakijaundwa bado?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hapo mwanzo Wizara yenyewe ilikuwa inahusika katika kudhibiti kwa kutumia Kitengo hiko cha EMAC, lakini baadaye kupitia Waraka Na. 4 ambao niliutaja kulikuwa kumeundwa Taasisi ya Elimu Tanzania ambayo kwa sasa ndiyo inashughulikia masuala hayo.