Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero ya nyani, kima, tumbili na ngedere kwa Wananchi wanaopakana na Mlima Kilimanjaro?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK ALOIS NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika,
Nakushukuru kwa kunipa tena fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Je Serikali ina mpango gani wa kushirikisha jamii ya vijiji vyote vinavyozunguka mlima Kilimanjaro ili kutunza rasilimali ambazo zipo katika mlima huo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Maporomoko ya Materu au Materu water falls iliyopo katika mto Kware katika viunga vya Mlima Kilimanjaro ni kivutio kikubwa cha watalii;

Je, Serikali ina mpango gani kusaidia juhudi za wananchi katika kuboresha maporomoko hayo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Patrick Alois Ndakidemi Mbunge wa Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, namna gani tunaweza tukawashirikisha wananchi; Ushirikisho wa kwanza ni kuendelea kuwapa elimu, kwa sababu tunaamini kwamba moja ya miongoni mwa mambo ambayo yanaweza yakahifadhi hili eneo au yakatoa huo ushirikiano wa kuwashirikisha wananchi au wanakijiji ni kuendelea kuwapa taaluma.

Mheshimiwa Spika, lakini cha pili ni kuanzisha na kuendeleza vikundi shirikikishi. Vikundi ambavyo vitasaidia katika kulinda haya maeneo. Lakini kingine, tumeona moja miongoni mwa njia ya kuweza kunusuru maeneo haya ni kuhakikisha kwamba tunawasisitiza wananchi wanaendelea kupanda miti kwa wingi. Kikubwa zaidi tunaendelea kuwaomba wananchi wa maeneo yale waache kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo yale ya Mlima Kilimanjaro, zikiweno shughuli za Kilimo, shughuli za ukataji miti lakini mwisho wa siku wanakwenda kuchoma miti pale na hatimaye inapelekea majanga makubwa. Kwa hiyo hiyo ni sehemu kubwa ambayo tumeichukua kama hatua ya kuwashirikisha wanakijiji.

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili katika suala la kuboresha na kutunza hichi chanzo cha maji cha Materu Water Falls, cha kwanza tunaendelea kutoa elimu kama kawaida yetu kwa sababu tuna amini elimu ndiyo itakayokitunza kile chanzo. Cha pili tumesisitiza watu waendelee kuipanda miti pale kwa sababu kisayansi miti ile ndiyo inayokwenda kuvuta mvua ile na tayari kile chanzo kina imarika. Kikubwa tunaendelea kusisitiza Wananchi wasifanye shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya vyanzo vya maji mwisho wa siku wanaharibu hivyo vyanzo.