Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiagize kuwe na madereva na kondakta wa jinsia zote kwenye mabasi ya shule ili kudhibiti vitendo vya ubakaji?

Supplementary Question 1

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza niwapongeze Serikali kwa kuchukua mikakati hii maalum kwa ajili ya kuwalinda watoto wetu. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali langu la kwanza, Je, ni hatua gani watachukuliwa ambao hawatatekeleza agizo hilo ama maelekezo hayo ya Serikali?

Swali langu la pili, kutokana na hali ilivyo sasa hivi hapa nchini kwetu na harakati ambazo wazazi na walezi tunazo, kuna umuhimu wa wale wasaidizi wetu ambao wanaishi na watoto wetu majumbani, kuwa na elimu ya ulezi wa Watoto. Mambo haya tayari yanafanyika duniani, ukienda Bara la Amerika yapo, ukienda Bara la Asia yapo, ukienda Bara la Ulaya pia yapo pia na Bara la Afrika kwa mfano, nchi za ya South Africa tayari wana training za child care kwa ajili ya kuwalinda watoto wetu waweze kupata malezi bora.

Je, ni lini Serikali itaanzisha vitengo hivi maalum, hata kama ikiwa ni VETA kuwafundisha wale Dada zetu wanaotoka maeneo mbalimbali ya Tanzania wanaokuja kufanya kazi majumbani ili waweze kupata hiyo training kwa ajili ya kuwalea watoto wetu kwa malezi yanayostahiki? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Najma Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza anataka kufahamu mkakati na hatua za Serikali itakazochukua kwa wale ambao watapinga utekelezaji wa waraka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, Serikali inaendesha taratibu zake kwa mujibu wa kanuni, sheria, taratibu na miongozo, kwa yule atakayekaidi au kupinga au kwa namna yoyote ile akakataa kutekeleza, basi sheria, kanuni na taratibu ndizo ambazo tutakazotumia kuhakikisha kwamba waraka huu unatekelezwa ili mambo yote yakae sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, anataka kufahamu mkakati wa Serikali juu ya namna gani tunafanya kwa wale wahudumu wa majumbani. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu Wizara ya Elimu kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi - VETA tumeanzisha kozi mbalimbali, sasa hivi tumeanza na hizi kozi za housekeeping ambazo zinafundisha hawa wahudumu wa majumbani au house girl na ma-house boy.

Naomba tuchukue ushauri huu wa Mheshimiwa Mbunge ni ushauri mzuri tuende tukaufanyie kazi tuweze kuangalia namna bora ya kuweza vilevile kuingiza kozi hii ya child care training kwa wale wahudumu wa majumbani. Ninakushukuru sana. (Makofi)