Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fedha zao waathirika wa Benki ya FBME iliyofilisiwa tangu Mei, 2017?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mbali na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa benki hii haikufilisika bali ilifilisiwa na inasemekana walikuwa na fedha za kulipa waathirika wa benki hii. Je, Serikali inajua maumivu wanayoyapata waathirika wa benki hii?

Swali la pili, kwa kuwa Serikali ndiyo dhamana wa mabenki yote Tanzania na Watanzania wengi wameathirika na benki hii. Je, haioni haja hivi sasa Serikali ikachukua jukumu la kuwalipa Watanzania wlioathirika katika benki hii na wao wakasubiri jibu la Mahakama? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Haji Mlenge kwa namna anavyofuatilia kwa karibu sana suala hili la benki ya FBME. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inajua kadhia hii na ndiyo maana Serikali inafuatilia kwa karibu sana siku hadi siku, mpaka kutoa wataalam wetu hapa kwenda kusimamia kesi hiyo kule Cyprus.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, naomba Mheshimiwa Mlenge uwe na subira mara tu maamuzi ya Mahakama yatakapotolewa na taratibu kukamilika nakuhakikishia kwamba Serikali itawalipa wateja hao bila pingamizi yoyote.