Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kushusha bei ya mbolea na pembejeo nyingine za kilimo ili kuongeza uzalishaji?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Kwa kuwa, mawakala ambao walitakiwa kutoa mbegu katika Jimbo la Arumeru Magharibi wamekataa kutoa mbegu kwa madai kwamba Serikali haijawalipa fedha zao na kusababishia wakulima kutopata mbolea katika maeneo husika. Je, nini kauli ya Serikali kwa ajili ya kuwasaidia wakulima hawa kwa haraka ili waweze kupata mbolea hasa katika msimu huu wa kilimo?

Swali la pili, kwa kuwa Mawakala hawa wanateuliwa na Wizara moja kwa moja kwenda kwenye Majimbo au Halmashauri.

Je, Serikali haioni sasa ifanye jambo la haraka kuwateua mawakala wa uhakika watakaokwenda kutoa huduma hiyo kwa wananchi hawa ili waendelee kupata huduma? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwamba Mawakala hawajalipwa fedha zao na ndiyo sababu ya kutokupeleka mbolea ya ruzuku kwa wananchi jambo hilo sidhani kama lina ukweli wowote, isipokuwa ni kwamba Serikali inafanya taratibu za kumalizia malipo kwenye baadhi ya Mawakala ambao watalipwa na kazi yao itafanyika, lakini kigezo cha kutokulipwa kwa sababu hiyo ni kigezo ambacho Serikali kupitia Wizara ya Kilimo haioni kama ni njia muafaka wa kuwasaidia wakulima na wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawataka Mawakala wote kutekeleza yale maelekezo ya mikataba ambayo walisaini kati ya Mawakala na Wizara ya Kilimo. Pia kuteua Mawakala wa uhakika jambo hilo tumelipokea na ndiyo maana katika awamu hii iliyofanyika, maana yake imetoa somo kwa Wizara ya Kilimo ambalo katika mwaka unaokuja maana yake itazingatia yale mapungufu yaliyojitokeza mwaka huu ili yasiweze kujitokeza katika msimu ujao wa kilimo. Ahsante. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kushusha bei ya mbolea na pembejeo nyingine za kilimo ili kuongeza uzalishaji?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa niombe radhi uliniita lakini sikuwa nimeuliza swali. Naomba niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa, kuna baadhi ya viwanda vinazalisha mbolea hapa nchini kikiwemo kiwanda cha Intracom pale Nara, kiwanda cha Minjingu na viwanda vinginevyo. Je, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba viwanda hivi na vinginevyo vinazalisha mbolea ya kutosha ili kuweza kukabiliana na upungufu wa mbolea nchini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA
KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kuleta wawekezaji wengi nchini ili waweze kuzalisha mbolea ya kutosha kwa ajili ya kusaidia usambazaji wa mbolea kwa wakulima wote nchini, ndiyo maana ukiangalia moja ya mwekezaji wetu ni hawa Intracom kutoka Burundi ambao wao watazilisha karibu tani 60,000 na moja ya mkakati mwingine wa Serikali ni kuhakikisha Minjingu inaongeza uzalishaji kutoka tani 30,000 mpaka tani 100,000 kwa mwaka. Lengo ni kuahakikisha kwamba wakulima wanapata mbolea zote kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondoe hofu huo ni mkakati wa Serikali na Serikali iko kazini kuhakikisha tunaongeza wawekezaji vilevile tunaongeza wigo wa viwanda vilivyopo kuongeza uzalishaji nchini. Ahsante sana. (Makofi)