Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza ajali zinazosababishwa na magari ya mchanga Wilaya ya Kaskazini B - Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini pamoja na kwamba takwimu haziko vema na ningeomba Mheshimiwa Naibu Waziri apate muda akajiridhishe na hizo data au takwimu zilivyochukuliwa, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa magari ya mchanga yanasababisha sana ajali za daladala pamoja na ajali za bodaboda hasa katika maeneo ya Kaskazini A Kule Nungwi na maeneo ya Donge kwa ujumla wake. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mpango gani wa kukaa na Wizara za Mawasiliano pamoja na Wizara husika kule Zanzibar ili kuweza kutatua tatizo hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa tatizo la magari ya mchanga kwenda mwendo wa kasi ni tatizo sugu hivi sasa. Je, Mheshimiwa Naibu Naibu Waziri haoni haja ya kukaa na taasisi inayoshughulikia masuala ya usafirishaji wa mchanga pamoja na maliasili isiyorejesheka ili kukaa na kuratibu utaratibu mzima wa leseni pamoja na utaratibu wa kusafirisha hizi rasilimali za mazao yasiyorejesheka? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Soud, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza takwimu hizi nimeletewa na Kamisheni ya Polisi Zanzibar, kwa hiyo nina Imani zimetoka kwenye mamlaka sahihi. Hata hivyo, kwa vile amesema tujiridhishe, mimi na yeye tutashirikiana kuzifuatilia, kama ana source nyingine yenye takwimu tofauti na hizi tutasaidiana kuona ni zipi ni sahihi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu magari haya kusababisha ajali kwa wingi kama alivyoeleza, kwa takwimu zetu kunaonekana kuna dalili ya kupungua. Hata hivyo, nieleze hata kama gari inabeba mzigo au ni mfanyabiashara na nini, anapoingia barabarani lazima azingatie Masharti ya matumizi ya barabara na kwa maana ya Sheria ya Usalama Barabarani inamhusu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu magari haya kusababisha ajali kwa wingi kama alivyoeleza, kwa takwimu zetu inaonekana kuna dalili ya kupungua, lakini nieleze hata kama gari inabeba mzigo ama ni mfanyabishara na kadhalika, anapoingia barabarani lazima azingatie masharti ya matumizi ya barabara na kwa maana Sheria ya barabarani inamhusu. Kwa hiyo, kwa hawa wanaobeba mchanga ninashauri nchi nzima siyo tu lile eneo la Mheshimiwa Soud alilolieleza kwamba, kwanza inatakiwa ule mchanga ufunikwe ili usitoe vumbi wanapokuwa wanaendesha yale magari. Pili wahakikishe magari yale ni mazima yanapoingia barabarani na madereva kwa kweli wawe sober enough wasiwe wamekula vilevi wakasababisha ajali kwa watu wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, tutaendelea kufuatilia kwa ukaribu na kupitia Bunge lako Tukufu nimwelekeze IGP kupia Kamisheni ya Polisi Zanzibar waimarishe usimamizi wa eneo hili lililobainishwa na Mbunge, eneo la Nungwi na maeneo ya jirani ili kukomesha kabisa ajari za namna hiyo. Nashukuru. (Makofi)