Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Abiria vya Bugorola, Ukara na Kisorya Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nishukuru kwa majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa kituo cha Bukimwi kinachopokea abiria kutoka Kayenze nacho vile vile hakina Banda kwa ajili ya abiria kusubiri usafiri. Je, ni sehemu ya vituo vitakavyofanyiwa ujenzi kama ilivyo Bugorola, Kisorya na Ukara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Kivuko cha kutoka Kitale kwenda Ilugwa na kingine kutoka Kakukuru kwenda Ghana ni vivuko vilivyoko kwenye maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi mwaka 2020 - 2025. Je, Serikali ina mpango gani kuanza ujenzi wa vivuko hivi kwa ajili ya kuokoa maisha ya wananchi kwenye eneo hilo? Nashukuru sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kwa awamu. Nikiri hivi vivuko alivyovisema viko kwenye ilani, lakini katika Ziwa Victoria tunajenga vivuko vipya vinne na katika Vituo vya Bukimwi – Kayenze vituo hivi kwa sasa haviko kwenye mpango wa kuvijenga kwa mwaka huu wa fedha labda kwa mwaka wa fedha unaokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vituo alivyovitaja vya Kitale – Ilugwa, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafahamu na tuna uhakika kadri idadi ya watu inavyoongezeka kuna haja kubwa sana ya kuongeza vituo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa visiwa hivi kwamba Serikali inafahamu na tunalifanyia kazi kutafuta fedha kuhakikisha kwamba tunakuwa na mawasiliano katika vile vivuko alivyovitaja vya Kitale, Ilugwa hadi Ghana, ahsante sana.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Abiria vya Bugorola, Ukara na Kisorya Ukerewe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. TEYA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika Daraja la Kijazi ile flyover ukipita inavutia na imenyooka, sasa ukiendelea kule mbele ukapita kwenye ile flyover pale VETA yaani sisi tunaoangalia inaonekana pale juu ukingo ule umepinda. Mheshimiwa Waziri, anasemaje kuhusu ile? Inaleta picha mbaya.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kama Serikali tuchukue na tuliangalie kama limepinda ama ni design, halafu tutakuja kulitolea majawabu kama tatizo lilikuwa ni usanifu ama tatizo lilikuwa ni Mkandarasi kama anachosema Mheshimiwa Mbunge kitaonekana kwamba kina mapungufu, ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Abiria vya Bugorola, Ukara na Kisorya Ukerewe?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mbeya ni jiji lakini hatuna stendi kubwa ya kutosha, stendi ile ni ndogo lakini hata taa haina. Je, ni lini Serikali itajenga stendi kubwa ya kutosha kwenye Mkoa wetu wa Mbeya? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu tulichukue kama Serikali na tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ambao hasa kwa kweli ndio wanaohusika na kujenga stendi hizi kwenye miji na majiji na kama TANROADS tutahitaji kusaidia, basi tutafanya hivyo ili Mkoa wa Mbeya hasa Jiji la Mbeya liweze kupata stendi kama alivyoomba Mheshimiwa Mbunge, ahsante.