Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: - Je, ni kero zipi za Muungano zilizoibuliwa na kutatuliwa toka kuasisiwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kuna msemo wa kisheria unasema, kwa tafsri yangu mimi, haki inayocheleweshwa ni haki inayonyimwa. Kwa kuwa mfuko wa pamoja wa fedha ni takwa la kisheria na ni muda mrefu sasa jambo hili linapigiwa makelele haujaundwa;

a) Je, ni nini commitment ya Serikali juu ya kuundwa kwa mfuko huu?

b) Je, ni lini Zanzibar itapata mgao wake wa hisa wa iliyokuwa East African Currency Board na faida katika Benki Kuu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO
NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu masuala mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa Mbunge wa Jimbo la Mtambwe. Kwanza nataka nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Khalifa amekuwa ni mfatiliaji mzuri wa masuala haya ya Muungano ambayo yanagusa mustakabali wa nchi zetu zote mbili. Mheshimiwa Khalifa hongera sana kwa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba moja miongoni mwa mambo ambayo hayajapatiwa ufumbuzi kama sehemu ya changamoto ni hili jambo la uundwaji wa hii kamati au Tume hii ya Pamoja ya Fedha. Tume hii ilikuwepo bahati nzuri imekwisha muda wake. Hata hivyo, sisi tayari tumeshapeleka mapendekezo kwa ajili ya kuteuliwa kwa tume hii. Nimwombe tu Mheshimiwa Khalifa awe na subra ili sasa tuzipe mamlaka zinazohusika zifanye uteuzi wa tume hii ili lengo na madhumuni sasa mambo haya ya muungano yaweze kwenda vizuri kama ambavo yanatakiwa kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu swali la msingi kwa upande wa swali la pili; ni kwamba changamoto hizi zilikuwa ziko nyingi, lakini kupitia Serikali hii ya Mama Samia Suluhu Hassan tumefanya juhudi kubwa kupitia kamati zilizoundwa za pande zote mbili. Kwa hiyo nimwambie tu kwamba huu mgawanyo ambao ameuzungumza unakwenda kupatiwa ufumbuzi na tutahakikisha kwamba tunafanya moja miongoni mwa jambo muhimu la utatuzi wa hii changamoto kwenye changamoto ama miongoni mwa haya mambo ya muungano.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: - Je, ni kero zipi za Muungano zilizoibuliwa na kutatuliwa toka kuasisiwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa kero za Muungano, ingawa Mheshimiwa Waziri hapa amejibu, anasema kwamba kero ya bandari imetatuliwa; lakini hadi jana nimepokea simu kutoka kwa wananchi ambao wamesafiri kutoka Zanzibar wamekuja Dar es Salaam na wamezuiwa mizigo yao midogo midogo bandarini. Nataka kujua, Serikali ituambie hapa;

Je, ni lini watalikomesha jambo hili na kero hii kuisha?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO
NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu suala la nyongeza la Mheshimiwa Asia Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika kikao chetu ambacho tulikaa tarehe 6 Disemba, 2022, miongoni mwa maazimio ambayo tuliazimia, kwa sababu kama nilivyosema kwamba suala la utatuzi wa changamoto za Muungano limeundiwa Kamati Maalum, kuna Kamati ya Wataalam, kuna Kamati ya Makatibu Wakuu lakini kuna Kamati ya Mawaziri. Kwa hiyo, mpaka tarehe hii tulipokaa tulikubaliana na tukatoa maelekezo kwa TRA na ZRA na Wizara zinazohusika kulifanyia kazi suala hili na kutoa mapendekezo ya ni kipi kinatakiwa kilipiwe na kipi ambacho hakitakiwi kilipiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge aendelee kuwa na subira, hili jambo tunalifuatilia na tunahisi tunapokwenda kwenye kikao kijacho tutalipatia ufumbuzi. Nawaomba Watanzania waendelee kuwa na subira, Serikali zote mbili zinazifanyia kazi hizi changamoto za Muungano.