Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Swali hili nimeliuliza mwaka 2020, 2021 na nikajibiwa majibu haya haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ametaja kwamba halmashauri ya Geita ina shule za sekondari tatu sisi halmashuri ya Geita tuna majimbo mawili, jimbo la Busanda na Jimbo la Geita. Shule mbili ziko jimbo la Busanda. Jimbo la Geita lina population ya zaidi ya watu laki saba na nusu, kwangu, tuna shule moja. Watoto wanalazimika kutembea kilometa 80. Sasa, bado nahitaji majibu sahihi ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kata ya Nkome ina wanafunzi 9500 ina shule nne; na miundo mbinu yote ya madarasa tumejitosheleza, tunapungukiwa tu ujenzi wa bweni kwa ajili ya kufungua kidato cha tano na cha sita.

Je Serikali iko tayari kupeleka pesa kwenye kata ya Nkome ili tuweze kufungua pia kidato cha tano na sita?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba majibu tuliyotoa kwa sasa ni sahihi kwa kuwa ni kweli Halmashauri ya Geita ina majimbo mawili, kwa maana ya Geita na Busanda ambao wana hizi shule za kidato cha tano na sita tatu. Ninajua mahitaji makubwa ambayo yako pale, ndiyo maana kwa sasa tumesema tunaendelea kuziimarisha ili kuongeza idadi ya wanafunzi wakati tunatafuta fedha kuhakikisha tunaongeza shule nyingine. Kwa hiyo nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali inapopata fedha itafanya hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu hii Shule ya Sekondari Nkome ambayo ina idadi kubwa ya wanafunzi na wanahitaji Bweni tu. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI niseme ombi hili tumelipokea na litafanyiwa kazi. Ahsante.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kakonko inayo shule moja tu ya kidato cha tano na sita, ambayo ni Shule ya Sekondari Kakonko, lakini tunazo Shule za Sekondari Nyamtukuza, Mhange, Shuhudia, Kasanda na Gwanum ambazo zina sifa, kwa maana ya kwamba zina madarasa lakini hatuna hosteli.

Je, ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya kujenga hosteli ili wanafunzi waanze kupokelewa kidato cha tano na cha sita? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Aloyce Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Kakonko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba mahitaji ya shule za sekondari kidato cha tano na sita yanapewa kipaumbele kwenye takriban majimbo mengi kwa sasa; na ndio maana katika jitihada zake Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutafuta fedha mliona, kwamba kwa kushirikiana na kampuni ya madini African Barrick walipewa dola milioni, takriban bilioni 70, ambazo ni kwa ajili ya ku-support elimu nchini. Fedha hizo zimeelekezwa katika ujenzi wa miundombinu ya kidato cha tano na sita. Kwa hiyo lengo la Serikali ni kuhakikisha hii adha inaondolewa. Kwa hiyo Mheshimiwa Kamamba nikuondoe hofu kwa sababu iko katika mipango ya Serikali.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Newala ina shule moja tu ya sekondari ya kidato cha tano; lakini inazo shule mbili ambazo zina sifa ya kuwa kidato cha tano, Shule ya sekondari ya Mpotola na Shule ya Sekondari Makukwe, lakini tuna shindwa kwa sababu hatuna mabweni au hosteli.

Je, ni lini Serikali itatuunga mkono kutujengea hosteli ili tuanze kidato cha tano na cha sita katika shule hizo mbili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda Mbunge wa Newala vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe hofu na yeye, kwamba Serikali imesikia na imepokea hayo maombi na itayafanyia kazi kwa kadri ambavyo tunatafuta fedha ili kuhakikisha wananchi wake wanapatiwa hiyo huduma ya kidato cha tano na sita na Watanzania wote kwa ujumla, ahsante sana.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusukuru kwa kunipa nafasi. Shule ya Sekondari ya Mkonoo iliyopo katika Jiji la Arusha ina madarasa kumi yaliyojengwa kwa fedha za uviko. Madarasa hayo yamekamilika na yana samani zote; lakini kwa sababu ya umbali madarasa haya hayajaanza kutumika hadi leo, takribani miezi sita sasa.

Je, Seikali haioni haja sasa kujenga hosteli kwenye shule hii ili madarasa haya yaanze kutumika? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa shule hiyo madarasa yameshakamilika na miongoni mwa halmashauri ambazo zina mapato makubwa ni pamoja na Jiji la Arusha. Kwa hiyo nimwelekeze tu Mkurugenzi wa Jiji kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa bweni hilo ili shule hiyo iweze kupata usajili na kusajiliwa kama ambavyo maombi ya Mheshimiwa Mbunge, ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 5

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa tatizo hili la uhaba wa hosteli katika shule za Serikali nchini limekuwa kubwa sana;

Je, Mheshimiwa Waziri haoni kuwa una haja kubwa ya kupeleka timu katika halmashauri zote ili kuratibu na kuona upungufu ulivyo mkubwa na hatimaye kuja kuiweka kwenye mipango ya Serikali?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimpongeze Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini kwa maoni ambayo ameyatoa. Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeyasikia na hivyo itayafanyia kazi kwa kuunda timu maalum ambayo itazunguka maeneo yote ili ipitie na kugundua ukubwa wa changamoto ambayo Waheshimiwa Wabunge wameeleza. Ahsante sana.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi. Shule ya Sekondari ya Busagara na Shule ya Sekondari Kumgogo zilizoko katika Jimbo la Muhambwe zina miundombinu ya madarasa kwa ajili ya kuanzisha kidato cha tano na cha sita.

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga hosteli ili tuweze kuanza huduma ya kidato cha tano na sita katika shule hizi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi Mbunge wa Jimbo la Mhambwe. Kama ambavyo nimeeleza hapo awali katika majibu mbalimbali ambayo nimeyatoa kwa waheshimiwa Wabunge, nimwondoe hofu kwamba sehemu ya timu ambayo itatumwa nafikiri itatumwa kupokea maoni yote ambayo Wabunge wote wameeleza; mapungufu katika shule ambazo tunaweza kuongeza aidha hosteli, bweni ama jengo la utawala na zikatumika kama kidato cha tano na sita zikiwemo za jimbo lako. Kwa hiyo waondoe hofu wananchi wa Muhambwe kwamba Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ipo kazi na itafanya kazi hiyo, ahsante. (Makofi)

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 7

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga hosteli katika Shule za Sekondari za Meatu na Kimali ili kuwapunguzia wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu kwa kifupi Mheshimiwa Minza Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshaeleza nia ya Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuongeza shule za kidato cha tano na cha sita nchi nzima ikiwemo katika Mkoa wa Simiyu. Kwa hiyo niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge wote kwenye dhana hii, kwa sababu fedha inatafutwa na sehemu ya fedha imeshapatikana ambayo itaelekezwa katika halmashauri zenu kwa ajili ya kuongeza mabweni sehemu zingine mabwalo ya chakula sehemu nyingine madarasa na vyoo ili tuweze kuzisajili na kuzifungua. Kwa hiyo hofu hiyo iondolewe kwa waheshimiwa wote.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 8

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kunipa nafasi. Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika inazo shule za Kalema, Kabungu pamoja na Bulamata, ambazo zina tatizo kubwa sana la ukosefu wa mabweni.

Je, ni lini Serikali watapeleka fedha ili waweze kujengewa mabweni?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti,ni kwamba Serikali bado inaendelea kutafuta fedha, na sehemu ya fedha ambayo imeshapatikana katika awali tayari kuna maeneo ambayo tayari imeshaelekeza kuhakikisha kwamba zinafunguliwa shule za kidato cha tano na sita na zianze kufanya kazi. Kwa hiyo hata haya maombi yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa yatawekwa katika mpango ili Serikali iweze kuyatekeleza kwa kutafuta fedha.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 9

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga hosteli katika Shule ya Sekondari ya Nasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu kama ifiatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa shule ambazo ziko katika mpango wa Serikali kuongezewa hosteli ni pamoja na shule ya Sekondari Ngaza ambayo Mheshimiwa Mbunge ameianisha hapo, ahsante.