Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini Shule za Sekondari za Lyamahoro na Rubale zitaanza kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kwa ajili ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa majibu hayo ingawaje kuhusu Lyamahoro Secondary School limejibiwa hivi zaidi ya miaka miwili, kwamba inaanza mwezi ujao, lakini haijaanza. Sasa swali: -

Je, Serikali inafahamu kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba nzima haina shule ya ngazi ya kidato cha tano na sita? Inafahamu hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Serikali inafahamu kwamba tukipata shilingi milioni 80 kila shule, kwa Lyamahoro 80 na Rubale 80, shule hizi zinakamilika kuwa na kidato cha tano na sita, zinaweza zikaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatambua shauku ya Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha katika Halmashauri yake ya Bukoba wanapata shule ya sekondari ya kidato cha tano na sita. Na ndiyo maana katika jibu la msingi Shule ya Sekondari ya Lyamahoro imeshapata sifa. Kwa hiyo, nimhaikishie tu kwamba Julai inapokuwa inaanza maana yake na shule hii itatekelezeka; kwa hiyo tunatambua kwamba hakuna na ndiyo maana utekelezaji wake unakwenda kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu kupeleka hizo shilingi milioni 80 katika hizo shule mbili ni sehemu ya fedha ambayo nafikiri itatosha tu kukamilisha baadhi ya miundombinu kwa sababu ili shule iwe na kidato cha tano na sita inahitaji bweni, bwalo, jengo la utawala pamoja na madarasa ya ziada na vyoo. Kwa hiyo kuna bajeti kidogo ambayo inahitajika kwa hiyo nimhakikishie tu kwamba Serikali itatafuta fedha ikishirikiana na halmashauri pamoja na yeye Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini Shule za Sekondari za Lyamahoro na Rubale zitaanza kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahasante sana. Shule ya sekondari Ifaru iko katika jimbo la Chemba mwanzoni ilikuwa na kidato cha tano na sita baadaye wakasitisha kwa sababu ya uchakavu wa miundombinu. Sasa uchakavu ule tayari Serikali imefanya ukarabati. Ni lini sasa itarejesha kusajili wanafunzi wa kidato cha tano na sita?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mohamed Monni Mbunge wa Chemba kwamba Ofisi ya Rais TAMISEMI imelipokea jambo hilo na italifanyia kazi; kwa sababu moja ya malengo ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ni kuhakikisha halmashauri zote nchini zinakuwa na shule za kidato cha tano na cha sita kwa sababu ya ongezeko kubwa la wanafunzi ambao wanawekwa sasa, kwa hiyo lipo katika mchakato na linafanyiwa kazi.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini Shule za Sekondari za Lyamahoro na Rubale zitaanza kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nimuulize Naibu Waziri swali dogo; Halmashauri ya Mji wa Bunda wananchi wamehamasika na wameanza ujenzi wa Sekondari mpya katika kata ya Nyamakokoto. Ni lini sasa mtamalizia majengo manne ya shule ya sekondari Nyamakokoto ili watoto wetu wa Bunda nao wapate nafasi ya kusoma vizuri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe hofu pia Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Mheshimiwa Ester Amos Bulaya ambaye amewazungumzia wananchi wa Bunda, kwamba moja ya malengo makubwa ya serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba shule zote ambazo zimeanza zinapata fedha na kumaliziwa. Kwa hiyo na hilo lipo katika mpango itapelekwa fedha kwa ajili ya kuhakikisha shule hiyo inakamilika.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini Shule za Sekondari za Lyamahoro na Rubale zitaanza kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Halmashauri ya Wilaya ya Hai tayari imeshapeleka maombi ya kupandisha hadhi shule nne kutoka kidato cha nne kwenda cha tano na sita, ambazo ni shule ya Lemila, Masikia, Longoi na Mkwasa. Je, ni lini Serikali itasajili shule hizi ili ziweze kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mafuwe Mbunge wa Jimbo la Hai kwamba Ofisi ya Rais TAMISEMI baada ya kuona shule zote zinakuwa zimeshakamilisha na kufikisha vigezo maombi ya usajili wa shule kuwa kidato cha tano na sita yanapelekwa Ofisi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kwa hiyo jambo hilo nafikiri lipo huko. Ofisi ya Rais TAMISEMI itashirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kuhakikisha jambo hilo linakamilika kwa zile shule ambazo zimekidhi vigezo.