Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutengeneza Bajeti kwa jicho la jinsia?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza hili suala sio jipya, limeanza toka mwaka 1997 kupitia TGNP, mwaka 2000 Serikali ikafanya mradi wa majaribio, mwaka 2010 kikaundwa hicho kikosi kazi anachokisema. Sasa kwa maelezo ya Waziri leo mwaka 2023 anasema kikosi kazi, maana yake anatuambia kwamba Serikali haiko serious, haijawa tayari bado kutimiza commitment zake za Mikataba ya Kimataifa iliyosaini? Kwa sababu sio jipya. Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa hili jambo ni la muda mrefu hamwoni sasa kwa mwaka ujao wa fedha 2024/2025 ni wakati muafaka kwa Serikali kupitia Wizara hii kuelekeza kila Wizara kuja na tamko la kijinsia katika upangaji na utekelezaji wa bajeti yake? Dhamira ni Serikali ama wananchi wajue kila shilingi iliyopangwa mwanababa amefaidika vipi, mwana mama amefaidika vipi, kijana amefaidika vipi, mlemavu amefaidika vipi? Ndio spirit ya hii concept. Sasa hamdhani kama Wizara ya Fedha...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mdee, uliza swali.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, Hawaoni sasa kwa mwaka ujao wa fedha 2024/2025, mwelekeze kila Wizara ije na tamko la bajeti la kijinsia?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Halima James Mdee, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza Serikali haiko serious? Naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko serious na tuko tayari kufanyia kazi masuala yote na maoni ambayo yanatolewa na Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, maoni yake tumeyachukua na tutakwenda kuyafanyia kazi. (Makofi)