Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Misamaha ya VAT inayotolewa inaleta tija kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ningeomba kuuliza maswali mawili madogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilitoa misamaha ya kodi ya VAT kwa taulo za kike na vishikwambi lakini tija haikuwepo kabisa. Je, Serikali inachukua hatua gani kukabiliana na changamoto hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa misamaha hii ya VAT kwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi imekuwa ikichelewa sana na inasababisha hata miradi ya maendeleo mingi kutokamilika kwa wakati. Je, Serikali inachukua hatua zipi kutatua kadhia hii? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Issa Mtemvu kwa ufuatiliaji wa misamaha hii ama harakati za ulipaji kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba misamaha ilitolewa kwa vishikwambi na taulo za kike lakini wako ambao walienda kinyume na taratibu lakini Serikali ilichukua hatua mbalimbali ikiwemo kufuta misamaha hiyo na kuhakikisha kwamba wafanyabiashara hao wamelipa kodi inayostahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili mikakati ambayo imechukuliwa na Serikali. Moja ni kubadilisha sheria, sheria iliyokuwepo zamani lazima Baraza la Mawaziri ndiyo litoe msamaha lakini kwa sasa iko juu ya Waziri wa Fedha na Mipango. Jingine Serikali imetengeneza mfumo ambao kwa sasa inaratibu misamaha yote hiyo na inatolewa kwa wakati.