Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwawekea mazingira mazuri Wakulima wadogo wa kilimo cha Umwagiliaji katika Mto Ruvu?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kwenye majibu ya Mheshimiwa Waziri eneo ambalo tayari limeshafanyiwa upembuzi yakinifu liko Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Morogoro Vijijini.

Je, Serikali haiko tayari sasa kuja kufanya upembuzi yakinifu kwenye Jimbo la Kibaha Vijijini kwenye Kata za Ruvu, Dutumi, Kwala, Gwata, Kikongo ili tuweze kuona namna bora ya kuwahudumia wakulima wadogo katika eneo hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Tunaposema wakulima kwenye Bonde la Ruvu ni wakulima wadogo, ni wadogo kweli kwa sababu wanatumia umwagiliaji kwa kutimia mashine ndogo na keni za mkono; na kuna katazo la watu kufanya umwagiliaji kwa kutumia Mto Ruvu. Je, Serikali inatoa tamko gani kuwasaidia watu wa Jimbo la Kibaha Vijijini kuendelea na umwagiliaji wa kutumia keni kwa kuwa hawajawa na mabwawa ya kutosha? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 20 Machi, 2023 tuliingia mikataba na washauri waelekezi kwa ajili ya kwenda kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mabonde 22 hapa nchini Tanzania likiwemo Bonde la Mto Ruvu. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika skimu alizizozitaja zitaingia ndani ya mpango huo wa Serikali ambapo kazi inaanza mwaka huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na katazo; kwa mujibu wa sheria inayoongoza matumizi ya maji na sheria za mabonde, imeweka utaratibu wa matumizi ya maji kupitia kibali maalum. Sisi kama Wizara tutakaa na wenzetu wa bonde kuweka utaratibu mzuri ili mwisho wa siku wakulima wetu wale wadogo walime kupitia taratibu zote za kisheria na kutunza mazingira pia. Kubwa zaidi ni kwamba tutaweka miundombinu mikubwa zaidi ili wananchi waachane na changamoto hiyo ya kubeba makopo kwenda kumwagilia.