Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y MHE. TOUFIQ S. TURKY aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa Saratani nchini?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Je, sasa Serikali ni lini itasaidia hospitali za Mikoa nazo kutoa huduma hii ya saratani, kwa sababu sasa hivi inatolewa katika Hospitali za Kanda tu na hospitali kubwa kama ile KCMC, Bugando na Ocean Road tu?

Swali la pili, kwa kuwa magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa ukiwemo ugonjwa wa kisukari, pressure pamoja na magonjwa mengine; Je Serikali sasa ina mkakati gani wa kutoa elimu ya kutosha hasa Wilayani ambako wagonjwa hawa ndiyo wanakotokea ili kuondoa rufaa nyingi kwa ajili ya hospitali kubwa kama Muhimbili?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ndiyo maana Serikali sasa hivi, Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha na amehakikisha hospital zote za Mikoa zina CT scan, maana yake sasa kwenye hospitali zetu za Mikoa wanaweza kucheki na kugundua mapema saratani kabla haijakua.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mkakati mahsusi wa kuwasomesha Wataalam kwa ajili ya kuwapeleka ngazi za Mikoa na kuweza kutoa huduma hiyo. Kwa sasa tunapima lakini tunashirikiana kwa kutumia telemedicine ili kuwasiliana na hospitali zetu za Kanda na Mikoa.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y MHE. TOUFIQ S. TURKY aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa Saratani nchini?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, saratani ya kizazi pamoja na saratani ya matiti imekuwa ni tatizo kubwa sana kwa wanawake. Je, nini mkakati wa Serikali wa kufanya utafiti wa kina ili kujua chanzo cha saratani hii ili iweze kuzuiwa badala ya kutibu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ndiyo maana umesikia kuna kampeni zinazoendelea kule shuleni na kwingine kuhakikisha kwamba watoto wanapata chanjo hasa watoto wadogo na wasichana, vilevile tunahamasisha sana kupima.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachukua ushauri wako na tutaendelea kufanya utafiti na kuona changamoto zinazosababisha mambo haya yaongezeke kila siku.