Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Arumeru?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; hospitali hii ni ya siku nyingi sana na majengo yake yamechakaa sana kiasi kwamba mengine yatalazimika kuvunjwa na kujengwa upya, lakini pia kuna changamoto ya eneo. Kwa Hiyo tunaona kwamba ni busara kuanza sasa kuwaza kwenda kujenga majengo ya ghorofa.

Je, Serikali pamoja na kwamba imetupatia shilingi milioni 900 ambazo tunashukuru sana, je, Serikali haioni kuwa ni muhimu kujipanga kwa ajili ya kujenga maghorofa kwa maana ya kwamba fedha ziongezwe? Hilo moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; hospitali hii haina
mortuary siku zote tangu imejengwa. Tumejitahidi tumejenga mortuary pale na mpaka sasa haijapata majokofu. Je, ni lini Serikali itatupatia majokofu ili ile mortuary ianze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hospitali hii ni kongwe, ni ya siku nyingi na mwezi mmoja uliopita nilifanya ziara pale nikishirikiana na Mheshimiwa Mbunge, lakini tulikubaliana kwamba kwa sababu imekwishaingizwa kwenye Mpango wa Hospitali Kongwe 31 kwa ajili ya ukarabati na upanuzi ndio maana mwaka wa fedha 2023/2024 imetengewa Milioni 900. Sasa dhamira ya kujenga hospitali mpya ndani ya halmashauri wanaweza wakakaa na kuleta mapendekezo Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili na sisi tuweze kuyatathimini na kuona kama yanaweza kutekelezeka ama vinginevyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, niwapongeze kwa kujenga jengo la kuhifadhia miili ya marehemu (mortuary) lakini jokofu liko ndani ya uwezo wa halmashauri kupitia Bohari ya Dawa (MSD). Kwa hiyo, nielekeze Mkurugenzi wa Halmashauri hii kuhakikisha kwamba wanaomba jokofu Kupitia akaunti ya MSD ili waweze kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Arumeru?

Supplementary Question 2

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali iliahidi kwamba imetenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Mbinga ambayo miundombinu yake imechakaa sana na ni hospitali ya siku nyingi. Je, ni lini ukarabati huo utaanza ili wananchi wa Wilaya ya Mbinga wapate huduma za afya bora na stahiki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bajeti ya Serikali ya 2023/2024 iliyopitishwa hapa Bungeni wiki iliyopita, Serikali imetenga Shilingi Milioni 900 kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali Kongwe ya Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Arumeru?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Je, ni lini sasa Serikali itajenga mortuary katika Kituo cha Malawi kilichopo Yombo Vituka Jimboni Temeke?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatvyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa uwezo wa mapato ya ndani ya Manispaa ya Temeke, naelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kuweka kipaumbele cha kujenga jengo la kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya cha Yombo Vituka, ahsante.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Arumeru?

Supplementary Question 4

MHE: YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha Afya cha Eshkesh kilipewa Shilingi Milioni 400 na imekamilisha jengo la OPD na nyumba ya Daktari, lakini bado jengo la Mama na Mtoto na kituo hicho hakijaanza kufanya kazi. Je, sasa ni lini Serikali itakamilisha jengo la Mama na Mtoto ili kituo hicho kianze kufanya kazi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Eshkesh kilipata shilingi milioni 400 na hatua za ujenzi zimefikia umaliziaji wa baadhi ya majengo na ni kweli kwamba jengo la Mama na Mtoto halijakamilika. Nimhakikishie tu kwamba Serikali iliweka mpango wa ujenzi wa vituo vya afya hivi kwa awamu. Tumekwenda awamu ya kwanza tumekamilisha majengo hayo, tunakwenda awamu ya pili kutafuta fedha kwa ajili kukamilisha pia jengo la Mama na Mtoto ili ianze kutoa huduma kwa wananchi, ahsante.