Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Watu Wenye Ulemavu mitaji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE.NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri.

Swali la kwanza, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia walemavu ambao hawajiwezi kujiunga na vikundi, kuwasaidia angalau baiskeli ya kutembelea?

Swali la pili; je, Mheshimiwa Waziri uko tayari baada ya Bunge hili tuongazane mimi na wewe kwenda kuwatambua walemavu walioko Mbogwe na kuwasikiliza shida zao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali wawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga Mbunge wa Jimbo la Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa au utaratibu wa mikopo ya asilimia kumi kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kundi la watu wenye ulemavu hawalazimiki kujiunga kwenye vikundi, hata mmoja anaweza akakopeshwa mkopo kama yeye na akafanya shughuli zake za ujasiriamali. Tayari wengi wameendelea kupata huduma hiyo kwa kupata mkopo kwa mtu moja mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na viti mwendo kwa watu wenye ulemavu utaratibu wa Serikali upo na maafisa maendeleo ya jamii katika maeneo hayo wanaainisha. Tunahusiana na wadau mbalimbali wanaendelea kuwasaidia. Kwa hiyo nitoe wito kwa halmashauri ya Mbogwe kuwatambua watu wenye ulemavu wanaohitaji viti mwendo ili Serikali iweze kuona namna ya kushirikiana na wadau katika kuwawezesha kupata viti mwendo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge hili la bajeti ili twende Mbogwe tuweze kupitia baadhi ya vikundi ambavyo vimenufaika, ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Watu Wenye Ulemavu mitaji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa kuwa Serikali imesimamisha kwa muda utoaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa mfumo uliopo mwanzo, na sasa hivi halmashuri hazitoi tena, ni lini serikali inakusudia kuleta hapa mwongozo wa utoaji mikopo hiyo ambao tutaupitia kwa pamoja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa
Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Constantine Kanyasu Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesitisha kwa muda utaoji wa mikopo wa asilimia kumi ili kupitia mwongozo vizuri ili kuhakikisha kwamba fedha ambazo zinakopeshwa zinarejeshwa lakini zinakuwa na tija zaidi kwa vikundi ambavyo vinakopeswa. Serikali iko kwenye hatua ya kuupitia mwongozo huo na mara utakapo kuwa tayari Waheshimiwa Wabunge wataufahamu.