Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuamua kuwa wasichana wasiolewe chini ya miaka 18?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Suala hili limekuwa lina muda mrefu sana, na watoto wanazidi kunyanyasika kwa kuolewa na umri mdogo; je, Serikali imejiwekea muda gani wa kufanya marekebisho hayo ya sheria?

Mheshimiwa Spika, swali labgu la pili; hivi hamwoni kwamba ipo haja ya kusitisha suala la maoni ya wadau, kwa sababu suala hilo ni wazi halafu hao wadau wengi ni hao hao wanaopenda kuoa watoto wadogo?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa majibu kwa swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, baada ya Mahakama ya Rufani kutoa maamuzi kwamba Serikali ibadilishe umri wa chini wa mtoto kuweza kuoa au kuolewa, Serikali ilileta mapendekezo hapa Bungeni. Bunge lako tukufu ndilo liliagiza Serikali ikachukue maoni zaidi kutoka kwa wadau mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, maelekezo hayo tumeyatekeleza, tumekamilisha na tuko tayari sasa kuja mbele ya Bunge ku-share maoni hayo pamoja na mapendekezo yaliyowekwa Mezani. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa, hapa Bungeni nyie mnapaswa kuleta Muswada. Ndiyo unamaanisha mko tayari kuleta Muswada? Kwa sababu maoni na mapendekezo, maana yake unayaleta kule ofisini, siyo hapa ndani. Sasa nataka nielewe vizuri, mnaleta Muswada au mnaleta hayo maoni na mapendekezo? Kwa maana maoni na mapendekezo hayawezi kuja hapa Bunge, hapa Bungeni tunasubiri Muswada.

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, tuko tayari kuleta Muswada. (Makofi)