Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka katazo la kisheria la kuswaga mifugo ili kuzuia uharibifu wa mazingira?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kupata majibu ya swali hilo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa utafiti uliofanywa na Tanzania National Carbon Center mwaka 2018 unaonesha kwamba mifugo ya kuchungwa – siyo ile ya kusafirishwa, ya kuchungwa inachangia asilimia 28 ya uharibifu wa mazingira. Je, Serikali ilitoa maagizo kwa halmashauri kwamba zitenge maeneo ya hao wafugaji ili wapate maeneo makubwa ya kufugia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, ranchi zetu zilizopo Tanzania haziwezi kutumika kama mashamba darasa ya wale wakulima wetu wakubwa wasiojua faida ya ufugaji ambao siyo wa kuswaga?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ninashukuru kwa maswali madogo mawili ya msingi ambayo Mheshimiwa ameyaeleza, nimhakikishie tu kwamba kwa sasa Serikali ina mpango wa kutenga maeneo na tumeanza kufanya hivyo, katika hatua ya awali mpaka sasa tumetenga hekta Milioni 3.38 ambazo zitachangia katika malisho na zimeelekezwa katika halmashauri za vijiji, lakini kutumia ranch kama eneo la mashamba darasa jambo hilo ndiyo lipo katika mkakati wa sasa na tumekuwa tukifanya hivyo katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, moja ya mipango mikubwa tuliyonayo Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni pamoja na hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameeleza. Ahsante sana. (Makofi)