Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Barabara hii imekuwa ikiahidiwa na viongozi wengi wakubwa wa Serikali tangu mwaka 2010 na haijatekelezwa mpaka sasa kwa kilometa hizo 148 kwa kiwango cha lami. Nini kauli ya Serikali kuikamilisha barabara hii kwa sababu imekuwa kero kwa watumiaji wake?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni lini pia Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kutoka Kahama – Nyandekwa – Nyamilangano (kilometa 148)? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Santiel Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo
– Bulige hadi Kahama ni kweli imekuwa ikiahidiwa na ndiyo maana tumeanza kuijenga kwa hatua na hasa maeneo ambayo tunajua ni ya mjini wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nia ya Serikali ipo na ndiyo maana tumefanya usanifu barabara yote na tumeanza kujenga maeneo yale muhimu kwa hatua tukitafuta fedha yote.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara aliyotaja ya pili kutoka Nyandekwa – Wogo, barabara hii ipo kwenye mpango na tumeipangia fedha kwenye mwaka huu wa fedha ikiwa ni maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Barabara ya kutoka Old Shinyanga kwenda Iselamagazi mpaka Solwa ni barabara ambayo inaunganisha Manispaa na Shinyanga DC.

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii tumeshaanza kuijenga kwa awamu na tunahakikisha kwamba tayari tumeshafanya usanifu na tutaijenga kwa kiwango cha lami ili kuunganisha Makao Makuu ya Mkoa wa Shinyanga na Halmashauri ya Shinyanga Vijijini. Kwa hiyo mpango upo kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Kiberashi – Chemba – Singida kandarasi yake imetangazwa lakini kuna kipande cha kama kilometa 18 kutoka Goima hadi Kondoa. Nataka kujua commitment ya Serikali ya kujenga kipande hicho. Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Goima – Bicha ni barabara ambayo sasa tumewaagiza Mkoa wa Dodoma waweze kufanya usanifu, maana yake ilikuwa haijafanyiwa usanifu, wafanye usanifu ili iwe ni link kati ya barabara ndefu ambayo tutaijenga ya Kiberashi – Singida halafu hiyo itakuwa ni link. Mwaka huu tumepanga waanze kufanya usanifu ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.