Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini barabara ya kilometa 0.8 kutoka Benki ya NMB hadi National Milling Kondoa Mjini itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nina swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, katika tengo la fedha hizi, je, Serikali itaweka pia na huduma ya taa za barabarani kwa sababu, barabara hii imekatiza katikati ya mji?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, ni mpango sehemu tunapojenga barabara za lami mijini tunaweka na taa. Na Mbunge atakuwa shahidi kwamba, mpaka sasahivi tumeshaanza kuweka taa za barabarani katika mji wa Kondoa.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini barabara ya kilometa 0.8 kutoka Benki ya NMB hadi National Milling Kondoa Mjini itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, je, ni lini barabara ya kutoka Itilima kwenda Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, Simiyu, ipo kwenye mpango na ndio maana sasa hivi tunachofanya ni kufanya review ya usanifu, ili Serikali iweze kujua gharama yake kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini barabara ya kilometa 0.8 kutoka Benki ya NMB hadi National Milling Kondoa Mjini itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika barabara ya Njia Nne hadi Kipatimu tayari Serikali imejenga kilometa 1.9 za lami. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha kilometa zilizobaki katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuikamilisha hiyo barabara kwa kiwango cha lami, lakini tutakwenda kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.