Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni shule ngapi za sekondari zimejengwa katika Mkoa wa Mtwara ambao una zaidi ya kata 50 ambazo hazina shule?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itajenga shule za sekondari katika kata ambazo wanafunzi wake wanatembea umbali mrefu kwa mfano Chilangala, Mkomatuu ambazo ziko katika Jimbo la Newala Vijijini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; tunafahamu na kutambua kwamba shule hizo zimejengwa tunashukuru, lakini mkakati wa kupeleka walimu ukoje kwa sababu shule hizo mpaka sasa haijapelekewa Walimu wa kufundisha? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la kwanza la je, ni lini Serikali itajenga shule hizi kwenye kata zilizosalia? Dhamira ya Serikali ni kujenga shule katika kila kata ya nchi yetu na hii ilikuwa ni awamu ya kwanza tu. Hata hivyo, niwatoe mashaka Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kwenda kwenye awamu ya pili ya kujenga shule hizi za kata na muda si mrefu wataanza kuona shule hizi zikijengwa katika halmashauri zote 184 katika nchi yetu. Kila halmashauri itapata walau shule moja kwenye awamu ya pili.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, Mkakati wa Serikali. Wabunge ni mashahidi, wameona namna gani Serikali hii ya Awamu ya Sita imetangaza ajira zaidi ya 21,000 kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Angela Kairuki ya kuajiri Walimu na watumishi katika Sekta ya Afya. Hii yote ni kwenda kuhakikisha kwamba Serikali inaziba mapengo haya ya Walimu ambao wanahitajika kwenye maeneo haya. (Makofi)

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni shule ngapi za sekondari zimejengwa katika Mkoa wa Mtwara ambao una zaidi ya kata 50 ambazo hazina shule?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, kumekuwa na idadi ndogo sana ya wanafunzi wanaosoma katika A-level Mkoani Mtwara. Je, Serikali haioni sababu ya kutoa motisha kwa kutenga kiasi kikubwa cha wanafunzi wanaotakiwa kusoma sekondari za A-level ambazo ziko katika Mkoa wa Mtwara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mchungahela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mkakati huo anaouzungumza yeye na ndio maana tayari imetengwa fedha ya kujenga shule za sekondari za mikoa kuhakikisha kwamba wanafunzi wanaotoka kwenye maeneo husika wanabaki katika maeneo hayo hasa wasichana. Pia tayari Serikali imekwishatenga Shingi Bilioni tatu kwa mikoa 10 ya mwanzo na sasa itakwenda tena kwenye awamu ya pili kwenye mikoa mitano, halafu itakuja kumalizika katika mikoa mingine, hii ni kuwabakiza.

Mheshimiwa Spika, vile vile kuna shule zile za A - level ambazo zilijengwa na wananchi kule na Serikali ikaja kumalizia, huwa zile zinatoa kipaumbele kwa wanafunzi wa maeneo yale kasoro zile shule maalumu tu za kitaifa ndio zinachukua wanafunzi kutoka katika kila eneo la Taifa letu. Naomba kuwasilisha.