Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu ya Hospitali ya Mji wa Bariadi?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa hii, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza nishukuru Serikali kwa kupeleka fedha katika majengo ya OPD na upasuaji lakini Hospitali ya Mji wa

Bariadi bado ina majengo mengi chakavu ikiwemo jengo la wagonjwa mahututi pia na majengo ya wodi;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuyakarabati ili yaweze kutoa huduma bora kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Hospitali ya Mji wa Bariadi ina changamoto ya upungufu wa wauguzi na madaktari; je, Serikali inatoa tamko gani juu ya upungufu huu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Hospitali ya Mji wa Bariadi ni hospitali kongwe na ndiyo maana Serikali iliona umuhimu wa kupeleka shilingi milioni 900 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa majengo ya upasuaji, na jengo la OPD. Zoezi hili la ukarabati na upanuzi wa hospitali ile ni endelevu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kila mara Serikali itakuwa inatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa hospitali kongwe basi Hospitali wa Mji wa Bariadi pia itapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kweli kumekuwa na upungufu wa watumishi wa sekta ya afya katika Halmashauri wa Mji wa Bariadi. Hata hivyo, mwaka uliopita Serikali ilipeleka watumishi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi la kupeleka watumishi kila kibali cha ajira kinapotoka Halmashauri ya Bariadi pia itapewa watumishi hao, ahsante.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu ya Hospitali ya Mji wa Bariadi?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi, naomba niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Matamba kinahudumia Kata tano za Kinyika, Matamba, Mlondwe, Itundu na Mfumbi. Kituo hiki kina zaidi ya miaka 30 hakijakarabatiwa.

Je, ni lini Serikali itakarabati kituo hiki ili kiweze kupata majengo mapya ikiwemo mochwari ambapo wananchi wanatumia Wilaya ya Mlale?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Festo Sanga Mbunge wa Jimbo la Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Matamba ni cha muda mrefu na ni tegemeo la wananchi kutoka katika kata takribani tano katika Wilaya ya Makete. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imekwishaainisha vituo vya afya vikongwe na chakavu na vyenye upungufu wa miundombinu kwa ajili ya kupeleka fedha kwa awamu kwa ajili ya kukarabati na kuvipanua. Kwa hiyo tutatoa kipaumbele pia katika kituo hiki cha Matamba kwa kadri ya bajeti ambavyo tunakwenda kuipanga; ahsante.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu ya Hospitali ya Mji wa Bariadi?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana. Pale katika Jimbo la Kinondoni kwenye Kata ya Kigogo Serikali ilituletea jokofu la kuhifadhia maiti lakini limekaa zaidi ya miaka mitatu sasa bila ya kuweza kujengewa eneo lake ilhali tathmini imeshafanyika;

Je, sasa Serikali imepanga kutoa lini fedha ili nyumba zilizokaribu pale ziweze kufidiwa na jengo lile likaanza kujengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Kigogo kilipelekewa jokofu lakini Serikali ilielekeza mara vifaa tiba vinavyofikishwa katika vituo vyetu vianze kutumika mapema iwezekanavyo. Kwa hiyo kwanza nitumie fursa hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha kwamba wanatenga fedha kwa ajili ya kujenga jengo la kuhifadhia maiti na kuingiza jokofu ili lianze kufanya kazi ya kuhudumia wananchi kama inavyotarajiwa, ahsante.