Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaajiri Wataalam wanaojitolea kwa muda mrefu kufanya kazi katika Hospitali mbalimbali nchini?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mahitaji ya watumishi wa afya nchi nzima ni 336,453; waliopo ni 114,582 sawa na asilimia 34 tu na pungufu ni 221,946 upungufu huu ni mkubwa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuajiri watumishi hawa ili kunusuru afya za Watanzania?

Swali la pili, Serikali haioni umuhimu wa kutengeneza database ili kutambua wahudumu wote wanaojitolea ili wakati wa ajira waweze kupewa kipaumbele? Ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Swali la pili: Serikali haioni umuhimu wa kutengeneza database ili kutambua wahudumu wote wanaojitolea ili wakati wa ajira waweze kupewa kipaumbele? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ni upungufu. Ni kweli tuna upungufu kwenye Sekta ya Afya na unachangiwa na mambo mengi. Wakati mwingine katika Hospitali ya Wilaya tumeweka idadi ya watumishi, Hospitali ya Mkoa tumeweka idadi ya watumishi, na Hospitali ya Kanda hivyo hivyo. Pamoja na hivyo, utakuta kwa mfano Hospitali ya Mawenzi wana watumishi 400 lakini pale Mwananyamala hospitali, wanaona wagonjwa 500 kwa siku; ukienda pale Mnazi Mmoja Dar es Salaam ambayo ni ya Wilaya wana watumishi 170 wanaona wagonjwa 700 mpaka 800 kwa siku. Maana yake ni nini?

Mheshimiwa Spika, tukienda kwenye eneo la kuangalia ni watu wangapi hospitali husika inaona wagonjwa kwa siku na tukaweza kupeleka watumishi kulingana na mzigo ulioko kwenye eneo, hata huo upungufu anaousema Mheshimiwa Mbunge haupo.

Mheshimiwa Spika, tulikwenda Wilaya moja kule Shinyanga wakasema wana upungufu katika Hospitali ya Wilaya. Nilipowauliza, wakasema tuko 37. Ni kweli ukiwasikia Hospitali ya Wilaya wako 37, utasema kwamba ni wachache sana, lakini nikawauliza mnaona wagonjwa wangapi kwa siku? Wakaniambia tunaona wagonjwa 13. Unaweza ukaona kwamba kuna umuhimu wa kufikiria. Hilo moja, ni kwamba linatakiwa lifanyiwe kazi, kuangalia hali halisi na kupeleka watumishi kulingana na mzigo.

Mheshimiwa Spika, la pili, lile la kuweka database, ndicho nilichokisema hapa, tutashirikiana na wenzetu wa Utumishi kuona namna nzuri tutakayofanya na kuweka database kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuwatambua wakati wa ajira wapewe kipaumbele. Hilo ni wazo zuri sana, tunalichukua na tunakupongeza Mheshimiwa Mbunge.