Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala ikiwemo na Halmashauri ya Mji wa Makambako?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

(a) Kwa kuwa, Serikali inakubaliana na mawazo ambayo wananchi wa Kijiji cha Mtewele na ndiyo wanahitaji kupata huduma Makambako kwa sababu kutoka Makambako kwenda kwenye Kijiji hicho ni kilometa nne tu na kutoka kwenye Kijiji kwenda kwenye Halmashauri yao ni kilometa 72. Je, Serikali inatuagiza nini ili tuweze kufanikisha wananchi hawa kwa sababu wako tayari kurudi Makambako?

(b) Swali la pili. Kwa kuwa Kata ya Kivavi ni kata kubwa sana na kwa sababu Serikali inania ya kuwahudumia wananchi jirani na maeneo wanakokaa. Je, Serikali itakuwa tayari tuanzishe mpango wa kugawa Kata hiyo ya Kivavi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu Kijiji hiki cha Mtewele kuwa kilometa Nne bado utaratibu ni uleule. Ni wao wenyewe kuanzisha mchakato sasa hapa inahusisha Halmashauri Mbili, kwa maana ya Wanging’ombe wakae kuridhia hili kwenye vikao vyao kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi na vilevile Halmashauri ya Mji wa Makambako nao waweze kupitia katika vikao vyao na waweze kuleta katika Ofisi ya Rais TAMISEMI ili mchakato huo uweze kuanza.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili nalo vilevile linafanana. Kata hii ya Kivavi kuigawa lakini nataka niongeze tu kidogo hapo. Kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuendeleza maeneo yale ambayo yaligawiwa hivi karibuni na tumeona jitihada kubwa ya Serikali ninyi Wabunge ni mashahidi. Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi sana kuhakikisha tunakamilisha majengo ya halmashauri, tunajenga nyumba za watumishi, tunajenga ofisi za Wakuu wa Wilaya. Kwa hiyo, kwa sasa kwanza kipaumbele kikubwa cha Serikali ni kuhakikisha tunaimarisha miundombinu kwenye maeneo ambayo yapo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala ikiwemo na Halmashauri ya Mji wa Makambako?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuiuliza Serikali. Ni lini wataukwamua mchakato wa kuupanua Mji wa Moshi ambao ulishapita ngazi zote alizozitaja ikiwa ni pamoja na kupata GN Na. 19 ya tarehe 15 Julai, 2016?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Tarimo, Mbunge wa Moshi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilimalizia kusema hapa, kwa sasa kipaumbele cha Serikali kwanza ni kuhakikisha tunakamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya maeneo ambayo yalikuwa yamekwisha megwa kupeleka huduma karibu ya wananchi. Baada ya hapo sasa tutaangalia mchakato huo mwingine wa kuweza kuendeleza maeneo kama ambavyo Mheshimiwa Tarimo amezungumza.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala ikiwemo na Halmashauri ya Mji wa Makambako?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Je, ni lini Serikali kwa kuwa mchakato wa kupata Halmashauri ya Bunda ulishatekelezwa na tulishaandika, sasa ni lini Halmashauri ya Jimbo la Bunda itapata Halmashauri kutokana na umbali wa kutoka kwenye Jimbo langu kwenda kwenye Jimbo lingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Getere, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, michakato kufika TAMISEMI yote tunaikusanya na kama nilivyoeleza hapo awali bado kwa sasa kipaumbele kikubwa cha Serikali ni kuhakikisha tunakamilisha miundombinu katika Halmashauri ambazo zilikuwa ni mpya na Wilaya ambazo ni mpya, baada ya hapo sasa tutaanza kuangalia tena haya maeneo mengine ambayo Mikoa imepitisha na kuleta kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais TAMISEMI.