Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzisaidia Kibajeti Taasisi za Wenza wa Viongozi Wakuu wa nchi ili ziweze kujiendesha na kupata ufadhili?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, swali langu linataka kufahamu kimsingi kwamba taasisi kubwa za nchi yetu, kwa maana ya Mahakama, Bunge na executive ya president, wale viongozi wakuu na wenza wao wanapokuwa madarakani wanaanzisha taasisi ambazo zinafanya makubwa katika nchi yetu. Taasisi hizo zinaaminika duniani zinapata fedha nyingi katika nchi yetu. Wanavyoondoka madarakani hakuna mfumo mzuri wa kiserikali wa kuziendeleza taasisi hizi. Kwa mfano Mkapa Foundation, WAMA, Tulia Trust leo inafanya makubwa lakini ukiondoka inapotea, Mama Magufuli alikuwa na taasisi ya wazee hatumwoni Mama Magufuli akiendeleza taasisi ya wazee.

Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Serikali viongozi hawa wanapotoka madarakani kuna utaratibu gani wa kuendelea kusaidia taasisi hizi kubwa kama nchi zilizoendelea, tunavyoona Jimmy Carter leo inaweza kuwa January Makamba. Ahsante.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, swali alilouliza Mheshimiwa Abubakari Asenga Mbunge ni swali zuri; lakini kwa kuwa hadi hapa tunapozungumza sasa hakuna sheria wala mwongozo wowote unaotutaka sisi kufanya kazi au kupeleka kibajeti juu ya hizo taasisi za wenza wa viongozi naweza kusema kwa namna moja au nyingine kwamba hatuna la kufanya kwa sasa hivi. Hata hivyo, kama mawazo yako yatakuwa mazuri tutaangalia, lakini kuchukua fedha za umma kupeleka kwenye taasisi za watu binafsi hili jambo halijakaa sawa.