Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je ni lini Serikali itatoa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo vya Kati nchini?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu hayo, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa mpaka sasa Serikali inatoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vitatu ambavyo ni vya Serikali MUST, DIT na Arusha Technical College ambao ni 2,435 pekee. Ni nini sasa maandalizi ya msingi ambayo Serikali imeshafanya mpaka sasa kuhakikisha kwamba inatoa mikopo kwa wanafunzi wote wa vyuo vya kati ikiwepo wa private? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa nini sasa Serikali isione namna ambavyo inaweza kushirikisha Sekta Binafsi ikiwemo benki ili na wao waweze kushiriki katika kutoa mikopo kwa vyuo vya kati kwa riba nafuu? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza anataka kufahamu maandalizi au mkakati wa Serikali kwa upande wa utoaji mikopo katika elimu ya kati. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, eneo la kwanza kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, tumeendelea au tutaendelea kupeleka ruzuku kwenye vyuo hivi vya elimu ya kati kwa lengo la kuhakikisha kwamba kwanza tunaenda kushusha zile gharama za uendeshaji au ile gharama ya ada ambayo wanafunzi wanalipa.

Mheshimiwa Spika, eneo la pili, tulilofanya kama Serikali, Serikali tayari imeshafanya mabadiliko ya Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ili kuhakikisha sasa tunaenda vilevile ku-cover elimu ya kati. Kwa hiyo ile Sheria ya Bodi ya Mikopo nayo tayari tumeshaifanyia marekebisho.

Mheshimiwa Spika, eneo la tatu, Serikali inafanya mapitio ya uwezo wa Bodi ya Mikopo namna gani inaweza kuratibu utoaji wa mikopo katika vyuo hivi vya kati.

Mheshimiwa Spika, eneo la nne kama mkakati Wizara sasa inafanya tathmini ya fani gani ambazo tutaanza nazo kwa ajili ya utoaji wa mikopo katika eneo hili la elimu ya kati.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili, anataka kujua mkakati wa Serikali kuhususha Sekta Binafsi, tayari tumeshaanza majadiliano na Sekta Binafsi ikiwemo mabenki na naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Benki ya NMB imetoa bilioni 200 kwa ajili ya mikopo hii ya Elimu ya Juu pamoja na kati na tunaendelea na juhudi hizo na wadau wengi wameonyesha nia ya kuunga mkono juhudi za Serikali.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.