Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba nifanye masahihisho kidogo, kituo kinaitwa

Rukalagata, Kata ya Biharamulo Mjini, kingine ni Kalenge Kata ya Kalenge na kingine ni Nyabusozi Kata ya Nyabusozi.

Mheshimiwa Spika, tarehe 9 Novemba 2022 nilisimama hapa ndani nikiongelea Kituo cha Rukalagata kwamba hakina jengo la upasuaji na bahati nzuri nikajibiwa na Waziri wa Fedha kwamba nilete maombi maalum na wao watanitengea pesa kwa sababu hospitali ya Biharamulo Mjini imejengwa lakini iko nje ya Mji kwa hiyo watu wa Biharamulo Mjini hawapati huduma. Barua yetu ilitoka Tarehe 14 siku tatu zilizofuata…

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa Ezra ni lipi?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Swali la kwanza je, hii barua ilishapokelewa na imefika kwa Waziri wa Fedha? Je, status ikoje, kama haijafika naomba niikabidhi hii barua.

Pili, napenda nishukuru kwa sababu nimeambiwa vituo viwili vitafanyiwa kazi. Ni hayo tu. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimepokea marekebisho, pili kwa kuwa barua iliwasilishwa na Halmashauri ya Biharamulo kwenda Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais -TAMISEMI tutafanya mawasiliano ya karibu na Wizara ya Fedha baada ya maswali hapa na tuone kama barua imeshafika na tuone hatua za utekelezaji ili ahadi ya Serikali ya kuleta fedha hiyo iweze kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, pili, hivi vituo vya afya viwili ambavyo vimetengewa shilingi milioni 500 ni vile kati ya vituo vya afya vitatu ambavyo Halmashauri mtaona kipaumbele ni vipi vianze ili tuanze kukarabati na kuanza kutoa huduma hizo. Ahsante. (Makofi)

Name

Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nami naomba niulize swali la nyongeza.

Je, katika hizo fedha shilingi bilioni 8.75 Kituo cha Afya cha Nkhomola kitakuwa ni miongoni mwa vituo vya kupatiwa hizo pesa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rose, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, fedha hizi ambazo zimetengwa shilingi 8,750,000,000 zitakwenda kuainisha vituo vya afya 20 vyenye uchakavu wa hali ya juu zaidi. Kwa sababu sina orodha hapa naomba kwa ridhaa yako baada ya kipindi hiki nitaangalia na kuona kama kituo hicho ambacho amekitaja Mheshimiwa kipo kwenye orodha hiyo, ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 3

MHE. JULIANA D SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru; wananchi wa Kata ya Sanga katika Wilaya ya Mbozi wamejenga boma la kituo cha afya; je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kituo hicho? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Sanga ambayo wananchi wamejenga boma kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya ni sehemu ya Kata nyingi kote nchini ambazo wananchi wamejenga, Serikali imeweka mpango mkakati, kwanza kukamilisha vituo vya afya ambavyo ujenzi wake umeanza lakini baada ya kukamilisha vituo hivyo tutakwenda awamu ya pili ya kuainisha maboma na kuanza kuyakamilisha na wakati huo tunatoa kipaumbele pia katika jengo hili la kituo cha afya cha Sanga, ahsante. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi; kwanza ninaipongeza Serikali imejenga vituo vya afya vingi sana ndani ya Halmashauri ya Tanganyika, tuna tatizo la ukosefu wa vitendea kazi kwenye vituo vya afya pamoja na watumishi.

Je, ni lini Serikali itapeleka vitendea kazi na watumishi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini, Kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba vituo vingi vya afya vimejengwa lakini katika mwaka wa fedha huu Serikali imetenga zaidi ya bilioni 193 kwa ajili ya kupeleka vifaatiba katika vituo vilivyojengwa. Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi kwamba kwa kiasi kikubwa vituo vyetu vimeanza kupokea fedha na vifaatiba kwa ajili ya kutoa huduma.

Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi hili litaendelea katika vituo vya afya vya Halmashauri ya Tanganyika. Ahsante sana.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 5

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; Zahanati ya Mongo la Ndege imejengwa kwa kipindi kirefu tokea nikiwa Diwani wa Ukonga.

Je, Serikali haioni sasa kutokana na ongezeko la wakazi kwenye mtaa wa Mongo la Ndege na maeneo jirani ya Jimbo la Segerea ni wakati sasa wa kupandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Zahanati ya Mongo la Ndege inahitaji kupanuliwa na kupandishwa hadhi kuwa kituo cha afya, kwa awamu hii tunaendelea kwanza na ukamilishaji wa zahanati na vituo vya afya ambavyo kazi ya ujenzi imeanza.

Mheshimiwa Spika, ninatoa wito kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuona uwezekano wa kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza kupandisha hadhi kituo hiki cha afya cha Mongo la Ndege. Ahsante. (Makofi)

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 6

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Uyui ambayo ndiyo kata kubwa kuliko kata zote katika Jimbo la Tabora Mjini haina kabisa kituo cha afya na tulikwishaomba muda mrefu ili iweze kupata kituo cha afya.

Je, ni lini Serikali itatupatia kituo cha afya katika Kata hiyo ya Uyui?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kata zote ambazo zina vigezo vya kujengewa vituo vya afya zitaingia kwa awamu baada ya kukamilisha vituo vya afya ambavyo vinaendelea kujengwa. Serikali imekwishatoa maelekezo kwa Halmashauri zenye mapato ya ndani yanayozidi bilioni tano, kuanza ujenzi wa vituo hivyo kwa kutumia ile asilimia 60 na asilimia 70 ya mapato ya ndani. Kwa hiyo, nitoe maelekezo pia kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kuanza kutenga fedha kwa awamu, wakati Serikali pia inatafuta fedha kwa ajili ya kupandisha hadhi lakini pia kujenga kituo cha afya katika kata hii, ahsante.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Kata ya Makanya katika Jimbo la Same Magharibi kimechakaa sana na ni cha zamani sana.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ili kukarabati kituo cha afya cha Makanya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Mathayo Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Makanya ambacho amekitaja Mheshimiwa Mbunge ni sehemu ya vituo ambavyo ni chakavu na Serikali inaendelea kuweka mpango mkakati wa kuvikarabati. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge aamini kwamba Serikali imetambua hilo, tunaweka mpango endelevu wa kukarabati na kituo hiki kitapewa kipaumbele. Ahsante.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Rugaragata, Kalenge na Nyabuozi – Biharamulo?

Supplementary Question 8

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Bweri ni kati ya vituo vya afya vya kwanza cha kwanza kujengwa pale katika Manispaa ya Musoma lakini hakikukamilika na kimechakaa sana pamoja na kituo cha Makoko.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha ili tuweze kuvimalizia vituo hivyo viwili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vedastus Manyinyi, Mbunge wa Musoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vya afya ambavyo Mheshimiwa Mbunge amaevitaja, kituo cha Bweri na Makoko ni sehemu ya vituo ambavyo Serikali inaweka utaratibu mahsusi kwa ajili ya kutenga fedha na kuvikarabati, vile ambavyo miundombinu haijakamilika vinatengewa fedha kwa ajili ya ukarabati na kujenga majengo hayo. Ahsante.