Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa REA III katika Wilaya za Busokelo na Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na idadi ya Vijiji ambavyo Mheshimiwa Waziri amevitaja, tunapozungumza Vijiji lakini Wakandarasi wamekuwa na tabia moja. Kwenye Kijiji anafika anaweka nyumba Tano au nyumba Nne na hapo anahesabu kwamba ni Kijiji.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuepusha hizi taarifa ambazo zinakuwa na mkanganyiko kwa Watanzania, unaposema Kijiji wakati ni wananchi wachache tu. Unapozungumza hili uwe umamaliza Kijiji chote?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na changamoto ambazo Wakandarasi wamekuwa wanashindwa kumaliza miradi yao kwa wakati. Wamekuwa wana sababu ya kutoa kwamba changamoto ni nguzo. Mheshimiwa Waziri tueleze leo, ni kweli Taifa letu lina changamoto ya nguzo?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimwia Aida Khenani, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika maeneo haya bahati nzuri Mheshimiwa Anthony Mwantona na Mheshimiwa Mwakibete suala hili katika masuala ya umeme katika Wilaya ya Busokelo na Rungwe wamekuwa wanakuja ofisini na kulizungumza na mimi na ni dhahiri kwamba katika mfumo wa awali ile scope ya kazi ilipelekwa karibu kilomita moja kwenye kila Kijiji.

Mheshimiwa Spika, taarifa njema ni kwamba Serikali imetafuta na kupata fedha karibu Dola Milioni 148 na tutaongeza na kupeleka kilomita mbili katika kila Kijiji. Kwa hiyo, maeneo yatakayopata umeme katika awamu inayokuja kwa kila Kijiji yatakuwa mengi zaidi na wanachi wengi zaidi watafikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu changamoto ni kweli kulikuwa na changamoto ya nguzo lakini imekwisha lakini changamoto kubwa zaidi ya kusuasua kwa miradi ni ile ambayo tumekuwa tunaizungumza ambayo ni kupanda kwa bei kwa gharama za vifaa vinginevyo ikiwemo waya za aluminum na copper bahati nzuri Serikali inalishughulikia jambo hilo kushirikiana na Wakandarasi lakini na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.