Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, natambua juhudi za Serikali katika kuendea suala zima la uwekaji mifumo ambayo itakuwa ni rahisi lakini utekelezaji ni mdogo sana na unachelewa sana. Andiko la Blue Print linaelekeza kwamba kutakuwa na mchanganuo wa jinsi gani ya kutekeleza na time frame.

Mheshimiwa Spika, swali langu, Je, Serikali iko tayari kuleta Bungeni mchanganuo wa jinsi gani changamoto hizi zinakwenda kutekelezwa na muda wake kwa maana ya time frame?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa Serikali ilidhamiria kujipima yenyewe kwa kutengeneza kitu kinachoitwa National Ease of Doing Business Report pamoja na kitu kinachoitwa Organizational Performance Index.

Je, Serikali imefikia wapi katika kutekeleza utaratibu huo? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo wawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimba Abbas, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayofanya katika kuhakikisha biashara na mazingira ya ufanyaji biashara hapa nchini yanakua.

Mheshimiwa Spika, ni kweli Blue Print utekelezaji wake ambao tulianza mwaka 2018 tunaenda vizuri lakini bado changamoto chache ambazo ni endelevu. Nakubaliana na yeye kwamba lazima tuhuishe kwa sababu changamoto zilizokuwepo wakati ule na sasa ziko tofauti. Kwa hiyo, tunahuisha time frame ya kuendelea kutatua changamoto za utekelezaji wa Blue Print kila mwaka na tutafanya taratibu hizo kuona Wabunge wote wanapata time frame hiyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu wa kuwa na National Ease of Doing Business, Wizara tumeanza kutekeleza hilo na hivi karibuni tutakuwa na vitengo katika Mamlaka za Halmashauri ambavyo vitakuwa vina Watalaam wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara ambao watashirikiana na Mamlaka ili kuhakikisha tunaendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, pia nichukue nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge ambao pia ni Madiwani tuendelee kushirikiana kwa sababu sisi ni sehemu ya Mabaraza ya Madiwani, tunapotunga zile Kanuni Ndogo (By Laws) basi tuangalie zisije zikawa nazo ni sehemu ya kuweka vikwazo vipya au kero mpya katika kutekeleza blue print. Nakushukuru.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi fupi kuuliza swali la nyongeza. Mifumo ambayo ni effective ni ile ambayo inatatua matatizo ya wawekezaji kwa muda na kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, hii blue print tumeisikia muda mrefu sana. Ni lini hasa itatoka au ni document nyeti? Tunaomba kauli ya Serikali kwenye hilo. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema blue print ni mfumo ambao unashughulikia au kurahisisha ufanyaji biashara hapa nchini. Tumeshaanza utekelezaji wake, hoja ya Mheshimiwa Mwanyika ni kwamba tayari kuna kero mbalimbali. Mwanzoni mpaka mwaka 2020 tulikuwa tumeondoa kero 232 lakini sasa tumeshafika 280. Lakini zaidi tumeshaanzisha mifumo ya kielektroniki ambayo inasomana kupunguza kero mbalimbali ambazo zilikuwa zimeainishwa katika matrix ile kwenye blue print.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaendelea kutekeleza hatua kwa hatua. Ninyi ni mashahidi kwamba sasa tumepunguza baadhi ya kero ile ya kupanga foleni kwenda kulipa kwa mfano katika taasisi mbalimbali tunatumia kielektroniki lakini pia moja ya changamoto kubwa ambazo tulikuwa tunazishughulikia ni miundombinu wezeshi ambayo Serikari ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan tunatekeleza barabara na miundombinu mingine ambayo tunaamini hiyo itaongeza ufanisi katika ufanyaji biashara na uwekezaji hapa nchini.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali moja la nyongeza. Pale Mjini Musoma kuna Mwekezaji aliyenyang’anywa kiwanda cha MUTEX kwa sababu ufanisi wake haukuwa mzuri. Serikali ikaahidi kwamba ndani ya muda mfupi tutapata Mwekezaji mwingine.

Je, ni lini sasa huyo Mwekezaji atapatikana kwa sababu ni zaidi ya miaka mitatu toka mwekezaji yule aondolewe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali tunahamasisha uwekezaji katika maeneo tofauti tofauti lakini Mbunge atakubaliana na sisi kwamba tayari kuna wawekezaji wengi sana ambao wameshaanza kuingia hapa nchini baada ya maboresho ambayo tunayafanya.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa tuna zaidi ya wawekezaji wa miradi 294 ambao wanategemea kuwekeza katika maeneo mbalimbali na tunategemea zaidi ya Bilioni Nane, Dola za Kimarekani ambazo zitawekezwa katika miradi hiyo ambayo tunaamini itaenda kutoa zaidi ya ajira 60,000.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Musoma nao katika eneo hilo la Mheshimiwa Mbunge miradi hii pia kwa kuwa tunashirikiana nae tutawasiliana tuone namna gani ya kuvutia wawekezaji hawa ambao wameonesha nia ya kuwekeza hapa nchini, waweze kuwekeza katika eneo la Musoma. Nakushukuru sana.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa biashara ya parachichi hivi sasa ni kubwa for export, na kwa kuwa biashara hii inafanywa zaidi na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikiwemo Mkoa wa Njombe pamoja na Mbeya.

Nataka kujua lini Serikali itaweka mfumo rafiki katika kuhakikisha kwamba wanaweka mfumo wa cold-room kwenye baadhi ya mabehewa ya TAZARA kama ilivyoainishwa kwenye blue print ili kuweza kuhakikisha kwamba parachichi zinafika Bandarini au Airport zikiwa na ubora? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli moja ya changamoto kubwa katika mazao au biashara ya matunda na mbogamboga ni hii mifumo ya cold-rooms ambayo ni changamoto kubwa. Sasa hivi tayari tumeshaanza kwenye ngazi za maeneo ambayo wanalima parachichi ikiwemo Njombe na Iringa kuwa na viwanda lakini pia na cold-rooms ambazo zitasaidia kutunza matunda hayo.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa hoja yake kwamba tuone sasa kwenye vyombo vya usafirishaji kwa maana miundombinu hii ikiwemo kwenye reli nao wawe na mabehewa maalum ya kuwa na cold-rooms ambazo zitasaidia kusafirisha parachichi ili zifike Bandarini au Airport kwa wakati bila kuharibika.

Mheshimiwa Spika, tunalichukua hilo wazo na tunalifanyia kazi kuhakikisha kwamba biashara hii inakuwa endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Supplementary Question 5

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Rais amefanya jitihada kubwa sana ya kuhamasisha wawekezaji kuja nchini. Mkoa wa Mwanza kuna eneo zuri sana na kubwa sana maeneo ya Nyamuhongoro lililopangwa kuwa industrial pack.

Je, Serikali ina mpango gani kuendeleza eneo hili? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli lengo la Serikali sasa ni kuanzisha industrial pack nyingi katika maeneo tofauti tofauti ikiwemo eneo hili la Mwanza. Katika Bajeti ya Mwaka huu tumeshaweka fedha kiasi kwa ajili ya kuanza kuweka maeneo haya ya industrial pack kwa ajili ya kuwezesha wenye viwanda kuwekeza katika maeneo ambayo yana miundombinu wezeshi ikiwemo majengo na barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunalichukua eneo hili pia la Mwanza ambalo ni muhimu sana kwa ajili ya kuwekeza viwanda nalo pia tutaliweka katika mipango ili kuhakikisha tunafikisha azma ya kujenga viwanda maeneo yote katika nchi yetu. Nakushukuru sana.